MAMA APORWA MTOTO

                        

Picha kutoka maktaba.

MWANAMKE mmoja mfanyabiashara ya samaki mkazi wa Kijiji cha Kaugeri Kata ya Mwaru Wilaya ya Ikungi Mkoa wa Singida Fatuma Juma (34) ameshambuliwa na kaporwa Mtoto wake wa mwaka mmoja na Salehe ambaye ni Mshikaji wake na Dereva wa pikipiki katika ugomvi wa kumgombania Mtoto na nyumba wanayoishi.

Wakizungumza  wakazi wa kijiji hicho Fadhili Juma na Hamisi Ramadhani walisema tukio hilo lilitokea juzi saa 1:00 usiku Mabandani Kaugeri kati ya Fatuma na Salehe wakimgombania mtoto na baadaye likajitokeza la kugombania nyumba wakati Salehe alimkuta Fatuma ana nyumba hiyo.

Wakazi hao walisema ugomvi wa watu hao wawili, Mama alikataa mtoto asichukuliwe kwanza ananyonya na bado mdogo ana mwaka mmoja tu lakini Salehe anadai amchukue kwa nguvu katika vuta nikuvute wakiwa mabandani Salehe akashirikiana na Hanje ambae ni Shemeji yake wakaanza kumshambulia Fatuma.

Habari zinasema watu hao wawili kwa pamoja wakaanza kumshambulia Fatuma kwa nguvu kwa kumpiga kwa nia ya kutaka kumpora mtoto hadi Fatuma akazimia masaa 10 akazinduka kituo cha afya Sepuka akipata matibabu.

Habari zaidi zinasema watu walikusanyika kuamua ugomvi huo kati ya Fatuma na Salehe wakawakamata Salehe na Hanje wakawapeleka ofisi ya kijiji kwa Mtendaji wa kijiji kwa mahojiano, Maelezo mengine ya ufahamu na maamuzi lakini watu hao waliachiliwa katika mazingira tata hivyo Salehe akapata nafasi ya kutosha akaondoka na mtoto hajulikani alikokwenda hadi sasa na mtoto alikuwa anaumwa.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa kijiji hicho Robert Afungwe anasema mkazi wake Fatuma Juma alipofika katika kijiji hicho miaka kadhaa ya nyuma alianzisha biashara ya kuuza samaki akapata eneo la kiwanja akajenga nyumba baadae akanzisha mahusiano na Salehe wakazaa mtoto mmoja ambaye sasa wanamgombania na imeelezwa Salehe tangu afike 2019 anakaa na Fatuma akiwa boda boda.

Polisi wa kituo cha Sepuka walimpokea Fatuma akiwa hoi amezimia kwa kushambuliwa na watu Wawili mtu na Shemeji yake wakampa hati ya matibabu kuenda kituo cha afya Sepuka na Mganga Mfawidhi wa kituo hicho. Dkt  Kessiah Mhina amethibitisha kumpokea Fatuma Juma akiwa hana fahamu amezimia na baada ya jitihada za waganga sasa anaendelea vizuri.


Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments