MSD YAENDELEA NA UTOAJI BORA WA HUDUMA YA AFYA MKOANI SINGIDA.

                                  

Omary Mosi Afisa Mauzo MSD kanda ya kati Dodoma Serikali kupitia MSD itahakiksha inaendelea kutoa huma ya dawa katika vituo vyote vya Afya nchini .



Mashine hii itatusaidia sana katika huduma za Upasuaji kwani tatizo kubwa lilikuwa ni Nishati ya Umeme Dr Anuar Mchaki.




Kituo cha afya kata ya Msange halmashauri ya wilaya ya Singida kimepokea mashine ya jenereta kutoka serikalini ili kuwezesha shughuli za matibabu kuendelea pindi inapotokea umeme kukatika.

Akipokea mashine hiyo Kaimu Mganga mfawidhi wa kituo hicho Anuari Mchaki ameishukuru serikali kwa kuwapatia mashine hiyo ambayo itawasaidia sana hasa nyakati za usiku kutokana na adha waliyokuwa wanaipata.

Dr. Mchaki amesema mashine hiyo itasaidia kuokoa maisha ya mama na mtoto ambao walikuwa hatarini kupoteza maisha kutokana na kukosa huduma muhimu hasa ya upasuaji inapotokea dharura.

Aidha mwenyekiti wa halmashauri hiyo na diwani wa Kata ya Msange Eliah Digha ameishukuru serikali na kueleza kuwa kituo hicho kina upungufu wa vyumba vya kulazia wagonjwa na pia wanaomba kujengewa jengo la X-ray ili wananchi wapate huduma kwa karibu.

 Naye afisa mauzo kutoka Bohari kuu ya dawa kanda ya Dodoma Omary Mosi akikadhi mashine hiyo amesema wana jukumu kubwa kuhakikisha dawa na vifaa tiba vinapatikana katika bohari kuu ya dawa ili waweze kuvihudumia vituo vya afya vya seriakli.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments