MADIWANI HALMASHAURI YA WILAYA YA SINGIDA WAJIPANGA KUMUONA WAZIRI WA NISHATI.

 Mwenyekiti wa Halmashari Mhe Elia Digha akifunga kikao cha Baraza la Madiwani la Halmshauri ya Wilaya ya Singida na kutoka na mkakati wa kukutana na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe Dotto Biteko.


Mkuu wa Wilaya ya Singida Muhandisi Paskas Muragili ajipanga kufanya ziara ya ukaguzi wa vyoo bora katika wilaya ya Singida ni katika utekelezaji wa agizo la Mkuu wa Mkoa  alilolitoa hivi karibuni.

                   

                                   Wajumbe wa kikao cha Baraza la Madiwani wakimsikiliza mkuu wa Wilaya.

                      



       Madiwani wakiwa katika kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi mpya wa ofisi za Halmashauri Ilongero.

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Singida  limeadhimia kuonana na Waziri wa Nishati Mhe Dotto Biteko Ofisini kwake Jijini Dodoma kwa Lengo la kutaka kuomba kuongezewa idadi ya  vitongoji vitakavyo patiwa umeme baada ya kupatiwa Vitongoji 15 tu kati ya Vitongoji 435 vilivyopo.

 Hayo yamejiri katika kikao Maalum cha Baraza la Madiwani kilichokaa kujadili na kupitisha bajeti ya Halmashauri kwa 2024/2025,  kilicho fanyika katika ukumbi wa ofisi za Halmashauri Ilongero.

 Wakijadili taarifa ya Mpango kazi wa Shirika la Ugavi wa Umeme nchini Tanesco Wilaya ya Singida iliyosomwa na Meneja wa Tanesco Eng Damas akisema kuwa kwa Mpango kazi wa Wilaya ya Singida ukiwa ni Vitongoji 15 tu ndiyo vitapatiwa Umeme pekee.

 Baada taarifa hiyo kutolewa na kuzusha mjadala ndipo Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe Elia Digha  na Baraza la Madiwani kukosa majibu sahihi kutoka kwa Eng Damas kwa pamoja kuamulu kuonana na Waziri mwenye dhamana ya Nishati Mjini Dodoma.

 Mhe Elia pia alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha tena Halmashauri kupata Shilingi Bilioni moja na nusu(1.5176b) kwa ajili ya kutekeleza miradi ya Ujenzi wa Madarasa(53) na Matundu ya Vyoo(160) huku  akiwataka Waheshimiwa Madiwani kuhakikisha wanasimamia ipasavyo matumizi ya fedha hizo ili Miradi  iweze kukamilika kwa Wakati na kwa Ubora.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhe. Paskasi Muragili ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Singida kwa kuongeza bajeti ya Halmashauri kutoka 1.4b mpaka 2.4b, amewataka Waheshimiwa Madiwani kuhakikisha wanasimamia  ukusanyaji wa Mapato kwani Halmashauri  inaweza kukusanya zaidi ya shilingi 3b na kuvuka malengo mliyojiwekea.

Akiitaja mikakati hiyo Mhe. Muragili ameongelea Mradi wa Vikundi vya Umwagiliaji ambapo tayari Maeneo Matano yanayofaa kwa shughuli hiyo yameainisha na takribani visima 50 vitachimbwa ili kuwezesha utekelezaji wa mradi.

Muragili amewaomba Waheshimiwa Madiwani kuiongezea nguvu Idara ya Ardhi kwa kutoa ajira za muda kwani nguvu kazi inahitajika katika Sekta ya Ardhi ili kuwezesha sekata hiyo kuwa na mchango kwenye Mapato ya Halmashauri.

Akihitimisha hotuba yake Mhe Muragili amewataka Waheshimiwa Madiwani kupokea Agizo la Mkuu wa Mkoa la kuwataka Wananchi wote wa Mkoa wa Singida kuwa na Choo Bora ifikapo tarehe 30/04/2024.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments