MMILIKI WA MIZINGA YA NYUKI AKUTWA AMEFARIKI.

                           

                                    Picha kutoka katika maktaba


MKAZI wa kijiji cha Nduluugu kata ya Ndulungu wilaya ya iramba Mkoa wa Singida mmiliki wa mizinga ya nyuki 3,000 na bustani ya mboga mboga na miti ya matunda eka 2 amekutwa amekufa kwenye kisima chake bustani kwake akioga. Juma Athumani (48) huku mwili wake ukiwa hauna nguo, viatu, simu nguo zake zikiwa juu ya tatu la kisima hicho.

Habari zinasema Juma Athumani (48) maarufu kwa jina la “Mabuku”alikutwa amekufa saa 4;00 na mdogo wake Saidi Athumani na mwili wake ukiwa unaelea juu ya maji ikidaiwa alifika hapo kwenye bustani yake kwenda kuoga kwenye moja ya kisima chake akitokea mnadani Sepuka Jumanne iliopita.

Saidi Athumani amesema juzi kuwa alikwenda kwenye bustani ya kaka yake kukagua kupata mboga na matunda saa 4:00 asubuhi kwanza akaiona na nguo zikiwa juu ya tuta, viatu na simu janja akajua anaoga lakini alipokaribia akauona mwili wa mtu ukiwa umeelea juu ya maji ya kisima hicho ni wakaka yake hapo hapo akili ikahama mahali pake,mapigo yakazidi nguvu akaanguka chini akapoteza fahamu akijua kaka yake amekufa saidi alichukua saa nzima nchini alipopata fahamu kidogo akautazama tena akapiga yowe la nguvu watu waliokuwa wakilima mbugani wapiti njia na wale wanaong’olea majani kwenye majaruba ya mpunga walisikia yowe wakafika kujua kuna nini kimetokea kwenye bustani ya mwenzao Juma Athumani walipofika na kumkuta Saidi analia mwili wa mtu ukiwa juu ya maji ukiwa hauna nguo wakatazama pikipiki, nguo,viatu na simu wakapata majibu ya maswali yao kwamba mwenye bustani hiyo na pikipiki hiyo amekufa na wao wakasaidia kupiga mayowe na kutoa taarifa kwa viongozi wa kijij na kata.

Mwenyekiti wa kijiji anasema amesikitishwa sana na kifo cha Juma Athumani “MABUKU” ambae ni mkazi wa kijiji chake mkulima na mmliki wa mizinga ya nyuki 3,00 yenye nyuki amepoteza maisha akioga kwenye kisima chake akitokea mnadani sepuka.

Viongozi wa kata walipofika na kushuhudia baada ya kupata taarifa hizo walisilikitika sana wanasema marehemu alikuwa mfano mzuri kwa wakazi wa kata hiyo alihamasisha ulimaji wa mboga mboga na utunzaji nyuki ili kuondikana na umasikini kirahisi kwa kutumia fursa zilizopo kwenye makazi ya watu.

Viongozi walitoa taarifa Polisi Ndangu na Kiomboi na walipofika walifuatana na waganga walifanya uchunguzi wa mwili wa Juma wakapata maelezo kutoka kwa saidi , viogozi wa kijiji ,wa kata wakaridhia kuwa Juma amefariki kisimani akioga na  Ndugu zake azikwe.  Kamanda wa polisi mkoa wa Singida kamishina msaidizi wa plisi ACP Stella Mutabihirwa hakupatikana kwa simu yake hata hivyo tukio kama hili ni la kawaida kutokea katika jamii.

Katika tukio jingine mifugo 20 imekufa kwa kupigwa na radi saa 11:00 jioni siku ya jumatano wiki iliyopita ikitoka machungani baada ya mvua kubwa kuanza kunyesha kwenye kijiji cha Nsonga  kata ya Kaselya wilaya ya Iramba Afisa mtendaji wa kijiji Remji John amesema mifugo hiyo  mali ya Athumani Mpondo ilikutwa na mkasa huo wakati ikirudi nyumbani jioni hata hivyo amesema radi mara nyingi hutokiea mara kwa mara kwenye eneo hilo.

Mwenyekiti wa kijiji Mujango Mdudi amesema mbuzi 5,kondoo 14 na ng’ombe 1 wamekufa kutokana na radi hiyo hakuna mtu aliyejeruhiwa hivyo familia yam zee Athumani Mpondo imepata hasara kubwa kwa kukosa mifugo 20.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments