IKUNGI YASAJILI WAKULIMA 12,989 KWENYE MFUMO WA MBOLEA.

 Mkuu wa mkoa wa Singida Peter Serukamba akiongea na viongozi wa ngazi mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi wakiwemo Madiwani wa halmashauri.


Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Thomas Apson akiongea kabla ya kumkaribisha mgeni rasimi Mkuu wa Mkoa.

Afisa Kilimo wa wilaya ya Ikungi Gurisha Msemo akitoa taarifa ya kilimo ya wilaya kwa Mkuu wa Mkoa Singida.


Viongozi wa ngazi ya Wilaya hiyo wakifurahia jambo katika kikao kazi hicho kilicho fanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi.

Wakulima wilayani ikungi wametawa kuhakikisha wanatumia vyema mbolea ili kupata mazao zaidi katika mavuno yao na kuinua pato la familia na Taifa.

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Singida Peter Serukamba wakati akiongea na maafisa ughani,madiwani na wakuu wa  idara mbalimbali kutoka ofisi ya Halmashauri ya wilaya hiyo.

Serukamba amewaagiza madiwani wote wilayani humo kwenda kufanya mikutano na wananchi kwa lengo la kutoa elimu juu ya matumizi bora ya mbolea.

Naye afisa kilimo wa wilaya hiyo Gurisha Msemo akitoa taarifa ya kilimo ya wilaya amesema kuwa wamefanikiwa kuongeza ekari za kilimo 15,261 ikiwa ni agizo la Mkuu wa Mkoa nakueleza kuwa  kuwa mpaka sasa halmashauri imefanikiwa kusajili wakulima zaidi ya 12,989 kwenye mfumo huku lengo likiwa ni wakuima 15,000 ambao watanufaika na mbolea hiyo.

Aidha mkuu wa Wilaya ya Ikungi Thomas Apson Amesema kuwa ili kufanikiwa na kutimiza malengo yeo lazima wakuu wa Idara na Viongozi wa ngazi mbalimbali wilayani humo lazima waungane katika kusimamia na kuendelea kutoa elimu kwa wananchi wa maeneo yote ili waweze kunufaika na matumizi ya mbolea.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments