BURUNDI NA RWANDA SASA WAANZA UPYA ?

 


Uamuzi mpya wa kufunga mpaka sio uamuzi pekee uliochukuliwa na Burundi. Waziri wa utawala na usalama nchini Burundi, Martin Nigetes, katika mkutano na mamlaka katika jimbo la Kayanza, alisema kuwa Wanyarwanda hawahitajiki nchini Burundi.

Akasema: “...Hatuhitaji watu wao wenyewe, na wale waliokuwa hapa kwenye ardhi hawatakikani”.

Warundi na Wanyarwanda waliozungumza  kuhusu uamuzi huu walionyesha kuwa ingawa mamlaka ya Burundi ina sababu za kuchukua uamuzi huu, wanaona kuwa ni hatua ya kurudi nyuma

Mwaka mmoja uliopita, Mrundi Aimé Claude Nkurunziza alianzisha upya biashara kati ya Kigali na Bujumbura kupitia njia ya ardhini, baada ya miaka mingi ya kutofanya kazi kwa sababu ya hali ya uhusiano kati ya serikali hizo mbili.

Wakazi mbalimabli wanaoishi jirani na mipaka ya nchi hizo mbili wakingea na vyombo mbalimbali vya habali wamesema kuwa:

"Mambo yalianza kwenda vizuri, sasa tazama. Hii haifaidi mtu yeyote, usalama ni sawa, lakini serikali zote mbili zinajali jinsi tunavyoishi. Nadhani haitakiwi kufungwa tena.”

Honorine Gatesi, anayeishi katika jiji la Huye kusini mwa Rwanda, pia anasema karibuni alianza kusafiri hadi Ngozi nchini Burundi kuwatembelea wanafamilia wake.

Aidha Honorine ameongeza kwa kusema kuwa “Sasa mimi pia nimenyimwa haki ya kuwatembelea binamu zangu, hawawezi kuja hapa na hatujui hii itachukua muda gani. Imepita zaidi ya miaka mitano tangu tulipowaona jamaa zetu mara ya mwisho. Ni jambo la kusikitisha.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments