WIZI WA MITA ZA MAJI WAZUA KILIO KATA YA KARAKANA (SINGIDA)

 

Mkurugenzia Mtendaji wa Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira Singida wa (SUWASA)
 Sebastian Warioba akiongea na wanahabari Ofisini kwake.





wananchi na wakazi wa Karakana Manispaa ya Singida wa sikitishwa na vitendo vya wizi wa mita za maji unaoendelea sasa.



SINGIDA:

Wakazi wa Kata ya Karakana, Manispaa ya Singida, wameibua kilio kwa Serikali na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (SUWASA) kufuatia wimbi la wizi wa mita za maji linaloendelea kushuhudiwa katika maeneo mbalimbali ya manispaa hiyo.

Wakizungumza na wanahabari, wakazi hao wamesema wizi huo umesababisha ukosefu wa huduma ya maji kwa muda mrefu, hali inayowalazimu kutafuta maji mbali na makazi yao. Wameomba hatua kali zichukuliwe haraka ili kukomesha vitendo hivyo.

“Huduma ya maji ikikatika kwa sababu ya wizi wa mita, maisha yanakuwa magumu. Tunahitaji suluhisho la haraka,” alisema mkazi mmoja wa Karakana.

Mkurugenzi wa SUWASA  Singida, Sebastian Warioba, amesema kuwa jumla ya mita 80 za maji zimepotea kutokana na wizi huo. Ameeleza kuwa mamlaka hiyo inashirikiana na Jeshi la Polisi kuwabaini wahusika.

Aidha, SUWASA imetangaza zawadi ya shilingi laki tano kwa yeyote atakayetoa taarifa zitakazowezesha kukamatwa kwa wahusika wa wizi wa mita hizo.

“Tunataka kushirikiana na wananchi kumaliza tatizo hili. Taarifa zote zitapokelewa kwa usiri mkubwa,” amesema Warioba.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments