MADIWANI 20 KUTOKA MUSOMA WATEMBELEA MANISPAA YA SINGIDA



Meya wa manispaa ya Musoma Mh Capten Mstaafu Wiliam Gumbo akiongea na Mtayalishaji wa kipindi cha Mtukio wa Standandard Fm 90.1 Singida Revocatus Phias maeneo ya Stend ya Misuna Singida mjini.
Jumla ya madiwani 20 na wakuu wa Idara kumi kutoka katika halmashauri ya manispaa ya Musoma wamefanya ziara ya kuitembelea halmashauri ya manispaa ya Singida ilikuona jinsi manispaaa ya Singida inavyo tekeleza miradi mbalimbali inayo fadhiliwa na benki ya Dunia.

Akiongea na standard redio Kepten Mtafu Wiliamu Patrick Gumbo ambaye ni meya wa manispaa ya Musoma amesema nao ni miongoni mwa halmashari kumi na tano inayotekeleza miradi inayofadhiliwa na benki hiyo.

Kapten Gumbo amesema katika vikao mbalimbali halmashauri ya manispaa ya Singida inasifiwa kwa kutekeleza miradi hiyo kwa  kiwango kinacho takiwa hali iliyowapa msukumo wa kuja kujifunza jinsi wanavyo itekeleza.

Amesema wametembelea miradi ya barabara zinazo endelea kujengwa katikati mwa mji huku wakitembelea stedi kuu ya mabasi ambayo amesema stendi hiyo ni miongoni mwa stedi bora nchini.

Katika hatua nyingine Kapten Wiliamu amewaomba wananchi katika manispaa ya Singida kujenga tabia ya kupisha miradi ya maendeleo kwani nifrusa katika kukuza uchumi wao na taifa kwa ujumla.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments