WANANCHI MKOANI SINGIDA WATAKIWA KUACHA TABIA YA KUJICHUKULIA HATUA MIKONONI KAMANDA


Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida ACP Debora Magirigimba

Wananchi mkoani Singida wametakiwa kuacha kujichukulia hatua mikononi dhidi ya wahalifu wanaokamatwa katika maeneo mbalimbali bali wawapeleke katika maeneo husika ilisheria ichukue mkondo wake.

Kauli hiyo imetolewa na kamanda wa jeshi la polis mkoani Singida Debora Magiligimba wakati akiongea na standard redio ofisini kwake kuhusu suala usalama katika mkoa.

Kamanda Magiligimba amesema kwasasa hali ya mkoa imeimarika kiusalama kutokana na ushiriki mkubwa wa wananchi kutoa taarifa kabala ya uhalifu na polis kufuatailia hatimaye kudhibiti mapema.
Aidha kamanda ameongea kuwa mbali nawananchi  kutoa ushirikiano mzuri limeibuka suala la wananchi kujichukulia sharia mkononi suala ambalo amesema ni kinyume cha sharia.


Katika hatua nyinge amesema jeshi la polis linataendelea kutoa elimu kwa wananchi katika maeneo mbalimbali ilikungeza ushirikia na jeshi hilo huku akiongeza kuwa ratiba yake ya kuzunguka katika nyumba za ibada kutoa elimu inaendelea.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments