FAIDA MALI YAENDELEZA MAPINDUZI YA KILIMO BIASHARA KWA VIJANA SINGIDA


 Katibu Tawala Msaidizi wa Huduma za Uchumi na Uzalishaji mkoa wa Singida Stanslaus Choaji akiongea baada ya kufungua Semina hiyo Mjini Singida.

Mwezeshaji kutoka Shirika la Faida Mali Muna Shabani akitoa maelezo mafupi juu ya Semina hiyo ya Siku Mbili.



Vijana kutoka wilaya za Mkalama,Iramba na Ikungi wakipatiwa mafunzo ya uwakala wa pembejeo za Kilimo,

SINGIDA

Na Cales katemana

Katika jitihada za kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana na kuwazuia kukimbilia mijini au kutegemea ajira za serikali, Shirika la FAIDA MALI kupitia Mradi wa YEFFA limeendelea kutoa elimu kwa vijana katika wilaya za Iramba, Mkalama, Ikungi na Singida ili kuwawezesha kujiajiri kupitia sekta ya kilimo.

Mratibu wa Mradi wa YEFFA, Munna Shabani, amesema mradi huo unatekelezwa katika mikoa ya Tanga na Singida, ukiwa na lengo la kuwajengea vijana uwezo wa kuzalisha ajira kupitia kilimo biashara, hususan katika mazao ya mboga mboga kama vitunguu, nyanya, migomba na mazao mengine ya muda mfupi yenye tija kubwa kiuchumi.

Ameeleza kuwa mradi huo unalenga vijana wenye umri kati ya miaka 18 hadi 35, na umekuwa chachu ya kuwainua kiuchumi kwa kuwapa mbinu bora za kilimo, usimamizi wa masoko, na namna ya kuongeza thamani ya mazao yao.

Aidha, Munna amewataka wauzaji wa pembejeo zaidi ya 200 waliopatiwa mafunzo juu ya ubora wa pembejeo kuhakikisha wanawauzia wakulima pembejeo halisi na bora, pamoja na kuzihifadhi kwa usahihi, ili kuongeza tija katika uzalishaji na kukuza kipato cha vijana wakulima.


Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments