Aidha
amezungumzia uchezaji wa klabu za Afrika katika Kombe la Dunia.
Kuhusu
hatua yake kukata nywele zake, amesema hilo halikuwa jambo la ajabu sana kwake.
"Ni jambo
nililokuwa nimelifanya miezi kama saba hivi iliyopita, lakini nafikiri mimi si
mzuri sana katika kuweka mambo mitandao ya kijamii - huwe siwezi selfie za
kutosha," amesema.
"Kwa hivyo,
ninajua ni jambo watu wengi hawajalizoea, kwa sababu nilikuwa na nywele ndefu
kwa miaka mingi - lakini kuwa bila nywele ndefu si jambo geni."
Amesema
hata hivyo kwamba "huwa inarahisisha mambo."
"Kwa
sababu sasa huwa situmii muda mwingi kwenye bafu," amesema Drogba
akihojiwa na BBC.
VIPI KUHUSU TIMU ZA AFRIKA URUSI
Mataifa ya Afrika
hayajapata matokeo ya kuridhisha Kombe la Dunia isipokuwa Senegal na Nigeria
ambao wameshinda mechi moja kila mmoja.
Misri na Morocco
tayari zimeyaaga mashindano na matumaini ni finyu kwa Tunisia baada yao
kushindwa 5-2 na Ubelgiji mechi yao ya pili.
Drogba anasema
Nigeria, mechi yao dhidi ya Iceland, walicheza jinsia anavyotaka kuona nchi za
Afrika zikicheza "kwa kushambulia, kutumia kasi na nguvu, na kushambulia
goli mara nyingi."
Anasema hilo
halikuwepo walipochapwa na Croatia mechi yao ya kwanza.
"Walikuwa
wanacheza wenyewe - kujiweka sawa, kujilinda bila kushambulia, na kwa kutoa pasi
sehemu moja ya uwanja hadi nyingine," amesema.
"Wakati huu (dhidi ya Iceland) walicheza
kushinda. Walikuwa na washambuliaji wawili na walikuwa na kasi sana na ukali
wakishambulia kiasi kwamba Iceland waliingiwa na asiwasi.
Walikuwa hawatabiriki
kwa mashambulizi na walivutia sana.
"Nilitarajia wacheze
hivi Kombe la Dunia - na ndio maana wakashinda mechi hiyo," anasema.
Anaongeza kuwa mataifa
ya Afrika yakicheza Kombe la Dunia yanafaa kudumisha utambulisho wao kama time,
na anasema ni Senegal pekee waliokuwa wamefanikiwa kufanya hivyo kabla ya
Nigeria mechi yao ya pili.
"Ni muhimu kwao
kuendelea kufanya hivyo - na Nigeria pia - ili wafike hatua ya 16 bora.
Wakiamua kucheza mchezo wa kujilinda na kuanza kuogopa kufungwa, watarudi
nyumbani."
0 Comments