HAPA KUTUMIA ZAIDI YA MILIONI 156 KUEKEZWA KATIKA UCHIMBAJI WA VISIMA VITATU IKUNGI, SINGIDA

 

Mkurugenzi wa Shirika la Health Action Promotion Assocciatin (HAPA) Seleman Dandy akiongea na wanahabari katika mradi wa maji katika kijiji cha Matyuku.


Meneja Mradi kutoka katika Shirika hilo Gerlad Nyamongoto akitoa maelezo mafupi juu ya Mradi huo

Meneja wa kampuni ya N&S Ground Water Tanzania Eric Poul akielezea namna wanavyotekeleza mradi huo katika kijiji cha Matyuku Wilayani Ikungi.



wamanchi kutoka katika kijijicha Matyuku kilichopo wilaya ya Ikungi wakitoa shukrani zao baada ya uwepo wa mradi huo.


SINGIDA

Shirika lisilo la kiserikali la Health Action Promotion Association (HAPA) limetangaza kuwa litatumia zaidi ya shilingi milioni 156 kwa ajili ya uchimbaji wa visima vitatu vya maji katika kijiji cha Matyuku, Wilaya ya Ikungi mkoani Singida.

Meneja wa miradi wa shirika hilo, Gerald Manyogoto, amesema mradi huo ni sehemu ya juhudi za kusaidia jamii kupata maji safi na salama, huku shirika likishirikiana kwa karibu na Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi kuhakikisha changamoto ya maji inapungua vijijini.

 “Tunafanya kazi kwa kushirikiana na serikali za mitaa ili kuboresha maisha ya wananchi kupitia miradi ya maendeleo. Maji ni moja ya kipaumbele chetu,” amesema Manyogoro.

Kwa upande wake, Eric Poul, Meneja wa kampuni ya N&S Ground Water Tanzania inayotekeleza uchimbaji huo, amesema kuwa tayari visima viwili vimekamilika na kazi ya kujenga miundombinu ya usambazaji maji itaanza hivi karibuni.

 “Kazi inaendelea vizuri, tunatarajia kuanza ujenzi wa miundombinu mingine ili wananchi waanze kunufaika na huduma ya maji,” amesema Poul.

Mkurugenzi wa shirika la HAPA, Seleman Dandy, amesema shirika hilo sasa linaendesha miradi saba ya maendeleo, ikiwemo afya, elimu, maji, usafi wa mazingira, utawala bora, mabadiliko ya tabianchi na ujasiriamali wa kijamii.

 “Tunataka kuona jamii ya Singida inakuwa na maendeleo ya kweli yanayogusa maisha yao ya kila siku,” amesema Dandy.

Mradi huu unatarajiwa kunufaisha mamia ya wakazi wa Matyuku na maeneo jirani, na ni sehemu ya dhamira ya shirika hilo kusaidia jamii kufikia maendeleo endelevu.

 Kwa habari zaidi kuhusu miradi ya maendeleo mkoani Singida, endelea kufuatilia ukurasa wetu!

#SingidaYetu #MajiNiUhai #MaendeleoVijijini  #HAPA #Ikungi #RadioSingida #VisimaVyaMaji #CommunityDevelopment #MajiSafinaSalama



Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments