MBARONI KWA KUFANYA MAPENZI NA MWANAFUNZI.

 


Ikungi

Na Mwandishi wetu

Mkazi wa kijiji cha mtunduru kata ya mtunduru  wilaya ya  ikungi  mkoani Singida Hamza  Hamisi (18) amekamatwa  na viongozi wa serikali saa 1:00 usiku nyumban chumbani kwake  akifanya mapenzi na Mwanafunzi  (14) ambae ni mwanafunzi wa kidato cha  pili (ii) .

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa juzi na mwenyekiti wa kijiji hicho Juma Nkambi  kuhusiana na tukio hilo amesema mwanafunzi huyo alikamatwa usiku mwishoni  mwa wiki iliyopita kwenye chumba cha Hamza wakifanya mapenzi kama kawaida yao huku Hamza akijua kuwa mwenzake ni mwanafunzi akitendo kitakacho pelekea kumharibia masomo na maisha na ndoto zake.

Mwenyekiti wa kitongoji cha Masweya Mashariki Alli Hamisi Lissu akiwa na Afsa Mtendaji wa kata ya mtunduru  Oska mwakakumbila walimkamata Hamza  usiku huo baada ya kupata taarifa za kiintelijensia wakiwa na Mwanafunzi huyo ana kwa ana chumbani kwake wakidaiwa kuvunja amri ya sita na wamekiri makosa yao.

Imeelezwa watu hao wamekuwa na mahusiano muda mrefu na wamekiri wenyewe kuwa na mahusiano baada ya kuhojiwa na polisi walipopelekwa kituoni na Afsa mtendaji wa kijiji cha mtunduru Veronika John wakiwa na baba wa Mwanafunzi huyo, mzee Martin Samweli.

Taarifa zinasema baada ya kukamatwa walifikishwa kituo cha Afya Sepuka  kwa  mahojiano na Mtoto huyo wa Shule  alifanyiwa vitendo vya kikatili  na Hamza yupo rumande na polisi bado wanaendelea na mahojiano na baadae  afikishwe kwenye vyombo vya sheria.

Mwalimu mkuu wa shule ya Sekondari Mtunduru  Epmat kairra amethibitisha kuwepo kwa taarifa hizo za mwanafunzi wake kukamatwa mitaani na kufikishwa polisi wakiwa na mshikaji Hamza Hamisi na mpaka sasa ameng’ang’aniwa na polisi kwa vitendo hivyo baada ya wote kukiri makosa yao walipokamatwa ana kwa ana na viongozi wa serikali.

Mapema mwaka huu waziri Mkuu Kassimu Majaliwa  aliwaonya vijana wote, wafanyabiashara na walimu kukaa mbali na wanafunzi wa kike wasikatishwe masomo yao na ndoto zao waache wasome akawaonya vijana yeyote atakayewakatisha watoto hao masomo watafungwa miaka 30 jela.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments