AMUUA BABA NA KUMFUKIA KWENYE TUTA LA VIAZI -SINGIDA.

 

Na Mwandishi wetu

KIJANA mmoja mkazi wa Kijiji cha Mwankoko “A” Kata ya Mwankoko Manispaa ya Singida mkoani Singida Athumani Jumanne (46) amemuua baba yake mzazi Jumanne Kivendi (71) katika ugomvi wa kifamilia.

Habari zilizopatikana kutoka Kijiji hicho zinasema tukio hilo lilitokea tarehe 30 Aprili 2024 saa 2:00 usiku wakati baba wa kijana huyo alikwenda kwake usiku huo baada ya kusikia mjukuu wake akilia akipigwa na Athumani, hivyo alikwenda kuuzima ugomvi huo.

Kwa mujibu wa habari zilizotolewa na Ayubu Ngura zinasema baba yake Mzee Jumanne alipofika kwa mwanae alianzaa kumfokea Athumani kwa maneno makali na matusi ya nguoni mbele ya familia yake.

Ayubu aliendelea kusema Athumani baada ya kusikia maneno makali na matusi kutoka kwa baba yake akakumbukia kuwa wana ugomvi wa ardhi wa mara kwa mara miaka ya nyuma baba huyo alimuua mkewe ambaye ni mama yake na Athumani na sasa anamtukana matusi ya nguoni mbele ya familia yake.

Aliendelea kusema baada ya matusi hayo Bwana Athumani alipata hasira na akamrukia Mzee huyo, akampiga ngumi mfululizo na kumwangusha chini na kumkaba koo kwa nguvu akaendelea kumshindilia ngumi akiwa chini mpaka alipokufa.

Habari zinasema baada ya mzee Jumanne kufariki mwanae alichukua jembe akaenda shambani kwenye eneo la jirani yake akachimba tuta akambeba baba yake akamtupia ndani ya tuta hilo, akachukua kiko chake akakiweka pembeni, akachukua majani ya n’gombe ba bati akaweka juu yake akafunika na siku ya tatu baadae akapanda miche ya viazi juu yake.

Baada ya siku tatu Athumani alikwenda kwa Mwenyekiti wa Kitongoji Nkingo akampa taarifa kuwa baba yake mzee Jumanne Kivendi hayupo nyumbani wiki tatu hajui alipo, ameondoka amechukua kiko chake na nguo zake mpaka sasa haonekani.

Imeelezwa siku ya 10 wananchi wa eneo hilo walitilia shaka wakaenda kwake kumhoji baba yake amekwenda wapi, majibu ya Athumani na maelezo yake, pia muonekano wake uliwatia shaka wakamuuliza kisa cha kulima tuta lile kubwa na kupanda miche ya viazi juu yake wakati eneo hilo sio lake la mtu mwingine ambaye ni jirani yake.

Alitoa majibu ya maswali hayo kuwa mke wa mwenye eneo hilo alimpa kibarua, mume wa mwenye eneo akamuuliza mke wake kwamba atampaje Athumani kibarua bila idhini yake, mke alikataa hapo wananchi waliondoka wakamuacha lakini minong’ono mingi chini kwa chini ilizidi.

Siku ya kumi na tatu saa 6:00 mchana wananchi wote wa eneo hilo walikusanyika wakaambiana wachukue jembe waende kwenye tuta hilo wafukue waone kuna nini, wakaanza kufukua, kwanza wakakutana na harufu kali wakaendelea kufukua wakaupata mkono wa kiko hapo hapo majibu ya maswali yao wakayapata na mtuhumiwa alikuwepo alipoona hayo akaanguka chini akazimia masaa mawili mbele ya Mwenyekiti wa Kitongoji na wananchi.

Wananchi wa eneo hilo la Mwankoko “A” wakaitana wote pamoja na viongozi wao na Diwani wao Imanuel Kiemi na Mwenyekiti wa Kijiji Bwana Yakobo Muve walifika kushuhudia tukio hilo, wakishuhudia nguo za mzee huyo, kiko na mwili wake ukiwa ukiwaq umezikwa kwenye tuta lililopandwa viazi juu yake, hapo hapo wakaita Polisi walifika kushuhudia tukio hilo na kulichunguza.

Imeelezwa Polisi wakifuatana na Madaktari kutoka Hospitali ya Wilaya ya Singida baada ya kazi ya ufukuaji wote kufanyika wakaanza kumhoji Athumani ilikuwaje mpaka amuue baba yake na alitumia kitu gani kuumua na kisa cha kumuua baba yaek.

Katika majibu yake alisema siku ya tukio hilo saa 2:00 usiku alikuwa nyumbani kwake akampiga mwanae Kivendi, babu yake kusikia kilio cha mjukuu wake alifika na kuanza kumfoka na kumtukana matusi ya nguoni akidai hataki mtoto huyo apigwe naama amepewa jina la ukoo wake hatakiwi apigwepigwe hovyo.

Athumani anasema baada ya matusi hayo makali akamrukia mzee huyo akampiga ngumi za ngumi kadhaa akamwaangusha chini akamkwida shingo akamkaba kwa nguvu akamkandamiza chini akaendelea kumpa kichapo akiwa chini baadae akamwacha.

Alipoona baba yake hawezi kuinuka, akiwa chini amenyamaza kimya kumbe muda huo alishakata moto alipoona hivyo akambeba akachimba shimo hilo akaweka bati na kiko akafukia shimo hilo na siku tatu baadae akapanda miche ya viazi juu yake.

Athumani ameendela kuliambia Jeshi la Polisi kuwa mara kwa mara walikuwa na ugomvi na baba yake wa ardhi eka moja na miaka ya nyuma mzee huyo alimuua mama yake mzazi.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kijiji cha Mwankoko “A” Yakobo Muve amesema Athumani ana mke na Watoto 4 na mji wake amekiri mbele ya Polisi na wanakijiji wenzake makosa yake yote na kuyatolea maelezo makosa yake mbele ya viongozi wake na wananchi, Polisi wakamchukua kwenda kutoa maelezo mengine kuhusiana na tukio hilo na wananchi wakaendelea na taratibu za mazishi.

Uchunguzi wa Jeshi la Polisi bado unaendelea juu ya tukio hilo.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments