YANGA YAENDELEZA UBABE SOKOINE MBEYA=NBC PREMER 2023/24

 

Timu ya Dar es Salaam ya Yanga imeedelea kupata ushindi katika dimba la Sokoine Jijini Mbeya katika mchezo wa ligi kuu Premer dhidi ya Wajerajera Tanzania Prisons fc ya Jijini Mbeya, katika Mchezo huo Prisons hawakuwa makini hasa katika eneo la ulinzi kwani walikuwa wakifanya makossa mengi hasa katika eneo lao ,Walionesha kujiamini kanakwamba wanacheza na timu yenye kiwango sawa na wao.

Ukiangalia hata goli la  Yanga la kuongoza limepatikana kutokana na kukosa umakini kwa viungo wa timu hiyo Jumanne Elfadhili,Lambart Charles Mussa Haji baada ya kupoteza muunganika wa tramision ya uanzishwaji wa mashambulizi,kwani viungo wa Yanga Mudadhiri Yahaya na Faridi Musa na Khalid Aucho walikuwa wametawala sana eneo hilo katika kipindi hicho cha kwanza.

Mpira wa majalo uliopigwa na Pacome Zouzoua ulimpita mlinzi Jumanne Elfadhili ambaye aliluka juu kuupigakichwa na kuukosa na kumkuta Clement Mzinze aliyekuwa nyuma yake na kuunganisha kimiani katika dk ya 8 ya kipindi cha kwanza huku golikipa wa prison Yona Amasi alishindwa kuudaka mpira huo.

Goli la pili la Yanga lilikuwa zuli pia  Prisons walifanya shambulizi langoni kwa Yanga bila kuwa na tahadhali kuwa iwapo mpira ukinaswa tunatakiwa tujilinde vipi,kama kawaida yake kiungo Khalid Aucho alipiga pasi ndefu ya pembeni kwa mlinzi wa kulia Yaw Kouassi aliyekimbia mita kadhaa na kupiga kross upande wa pili mpira uliyomkuta Pacome Zouzoua na kufunga goli la 2 katika  Dk 45+4 likiwa ni goli lake la 5 katika msimu huu.

Kipindi cha pili mwalimu wa Prison fc Hamad Ally alifanya mbadiliko katika eneo la kiungo Ally Msengi aliingia kuchukua nafasi ya Mussa Haji jambo ambalo liliongeza uhai kwa Prison,mabadiliko hayo yaliifanya Yanga kukosa uhai na muunganiko zaidi na kumfaya Khalid  Aucho kufanya kazi ya ziada,Dk 58 kipa wa Yanga Metacha Mnata alipewa kadi nyekundu kwa kumchezea vibaya Samson Mbagula na mwamuzi wa mchezo huo Alajiga kumpa kadi nyekundu.

Bao la kufutia machozi la Prison limefungwa na Jeremia juma baada ya mpira wa adhabu iliyosababishwa na Metacha mpira ambao ulikwenda moja kwa moja kimiyani na kumujacha gorikipa wa Yanga Abutwalib Mshery aliyengia kuchukua nafasi ya Metacha Mnata kushindwa la kufanya,

Pamoja na Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika uwanja wa ugenini lakini bado mwalimu gamondi anatakiwa kuendelea kuiweka sawa timu hiyo kutokana na inavyocheza sasa,Prisons kama wangekuwa makini wangeweza kupata bao la kusawazisha huku Yanga kwa asilimia flani wameonekana kuwa na upungufu katika maeneo flani.


Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments