(picha kutoka maktaba yetu)
MGANGA MKUU wilaya ya
Ikungi Mkoani Singida (DMO) Dkt Dorisilla ameahidi kuipambania afya wilaya ya
Ikungi kwa watu wote kwa kuanzia ukamilishaji wa ujenzi wa majengo ya Zahanati
vituo vya afya, Hospitali zake na upelekekali wa vifaa tiba na dawa sambamba na
watumishi.
Licha ya kuwepo kwa changamoto
mbalimbali kuwepo vituo vya kutolea huduma za kiafya kwa wananchi serikali
itaendelea kuziondoa moja baada ya nhingine ili wananchi wapate huduma zote za
kuafya kwa ukaribu zaidi kwa viwango vinavyotakiwa na taifa.
Mganga mkuu Dkt Dorisilla ameyasema
haya katika makabidhiano ya gari mpya la pili la wagojwa kwa viongozi wa
serikali na chama cha ccm na uongozi wa kituo cha afya Sepuka.
Dkt Dorisilla amesema gari hili lenye
thamani ya zaidi ya shilingi milioni 190/= litatumika kupunguza vifo na wa mama
wajawazito na watoto kwa muda wote na ndio hasa malengo ya serikali ya Rais
Samia hata hivyo Mganga huyo amefurahishwa kusikia wananchi wameridhishwa na
huduma za kiafya zinazotolewa na watumishi wa kituo hicho.
“Mambo mengi serikali awamu ya sita
ya Mama Samia imeyafanya kwa wananchi wake nchi nzima kwa kusogeza kwa ukaribu
huduma zote muhimu kwa wananchi hivyo sisi watumishi wa afya tunampangeza sana
Rais wetu Mama Samia “MAMA ENDELEA KUTUPIGANIA SISI WATOTO WAKO”.
Dkt Dorisilla ameendele kusema sasa
nchi nzima wameanza kumuelewa vizuri Rais wao Samia anataka nini kwao na si
hivyo tu na viongozi nao wameanza kwenda na kasi anayoitaka Rais Samia.
DMO Ikungi amewataka akina Mama
kukitumia kituo hicho kupata huduma za kiafya zenye uhakika tofauti na mwanzo
ambapo akina Mama watumia muda mwingi kupata huduma za waganga wa kienyeji.
“Tiba hizo hazina uhakika
huchelewesha muda na mwishowe watu wanapoteza maisha kwa tatizo ambalo
lingemalizwa na vituo vya kutolea huduma za kiafya vilivyopo kwenye maeneo ya
watu”.Alisema DMO kwa upande wake katibu wa mbuge wa jimbo la Singida Madgaribi
Abubakari Munna ameishukuru serikali ya mama Samia kutoa gari jipya la wagojwa
kwa ajili ya kutoa huduma za usafiri kwa wananchi tarafa ya sepuka na vijiv vya
jirani wilaya ya Iramba nah ii ni kwa sababu serikali yake iko karibu na
wananchi wake muda wote.
Mganga Mfawidhi wa kituo cha afya
Sepuka Dkt Kessiah Daniel amesema kituo chake kinatoa hudumd za kiafya muda
wote na kwa wananchi wote na huduma hizo wananchi wanaridhika japokuwa bado
kuna changamoto chache bado zi-po hasa umeme kukatika katika mara nyingi kwa
masaa mengi hata hivyo serikali inalijua hilo.
Dkt Kessial anasema katika miaka ya
nyuma kituo kilipoanza kilikua kinapokea akina Mama 14 tu kwa mwezi lakini sas
kituo kinapokea akina mama 70 kwa mwezi baada ya huduma zake kuboreshwa na kuwa
na watumishi wazuri wanaijituma na wenye ujuzi na kazi walizopewa na serikali.
Ameendelea kusema idadi hiyo
itaongezeka siku zote hasa baada ya kituo cha afya kufikia malengo yake katika
baadui ya majengo yake na wataalamu kuongezeka kusimamia idara zao muhimu
watakzo pewa na malengo hasa ya kituo ni kupambania afya wananchi sepuka.
“Gari tulilopewa na serikali ya
Rais Samia Suluhu Hassani litapinguza sana vifo vya akina Mama wajawazito na
watoto hawatazalia njiani wala wakunga wa jadi hawatatumika kuzalisha akina
Mama majumbani litawawapeleka wagojwa na akina mama wajawazito kwenye Hospitali
kubwa kwa matibabu”
Diwani wa kata ya sepuka Halima
ng’imba (ccm) aliishukuru serikali ya Rais Samia kuwajali wananchi wa tarafa ya
Sepuka kwa kutoa gari mpya ili zitoe huduma kwa wagojwa wa kata yake, tarafa na
vijii vya jirani vya wilaya ya Iramba amewataka waganga wasimamie vizuri
majukumu yao ili wagonjwa wapate matibabu yanayostahili na wananchi waiamini
serikali yao walioichagua.
0 Comments