MAKAMU MWENYEKITI UVCCM TAIFA Ndg. REHEMA SOMBI(MNEC) AFUNGUA TAWI BABATI VIJIJINI

 



Ndg Rehema Sombi Afungua Tawi la wakereketwa kikundi cha Nguvu Kazi Bodaboda kata ya Mwada wanufaika wa Pikipiki 5 kutoka kwenye Aslimia 4 za Halmashauri zinazotokana na mapato ya ndani, amewaeleza Madhumuni ya Ziara kwamba ni kuangalia Uhai wa Chama na Jumuiya zake, Kukagua Utekelezaji wa Ilani2020-2025 na Kuhamasisha Ushiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa2024.

Na Kazi yetu nyingine kama Umoja wa Vijana wa CCM ni kubaini Talanta za Vijana na Kuwasaidia kufikia malengo kwa kuwatengenezea mazingira Rahisi ya Kuonyesha na kunufaika na Taranta zao.

Nao Bodaboda wa kata ya Mwada, Babati Vijijini Mkoani Manyara waomba Chama cha Mapinduzi kiwape kipaumbele Vijana Katika kushiriki uchaguzi wa serikali ya mitaa 2024. Hayo yamesemwa mbele ya Makamu m/kiti UVCCM Taifa Ndg. Rehema Sombi alipofika kufungua Tawi la Wakereketwa kwa kikundi cha nguvu kazi.

Pia Amefikisha Salamu na Zawadi ya Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Dr. Samia Suluhu Hassan kwa Mamalishe wa Babati Vijijini kwa lengo la Kuthamini mchango wao katika Kukuza na Kujenga Uchumi wa Taifa, na amenipa zawadi hii ya vazi la mgahawani(Apron na kofia) niwaletee zenye ujumbe usemao( Shiriki Uchaguzi kwa Uadilifu) .

Pia niwakumbushe kuchangamkia Fursa ya Mikopo ya Halmashauri pindi itakapoanza kutolewa upya. Aidha ametembelea Shule ya Sekondari Mbugwe na Kusomewa Utekelezaji wa Ilani ya CCM 2020/2025 kwa Kujengewa Madarasa, Madawati na Bwaro la Chakula pamoja na kutoa Shukran za Dhati kwa Dr. Samia kwa Fedha za kukamilisha miradi hiyo. Hivyo Ndg. Rehema Sombi amewasisitiza Wanafunzi wa Sekondari ya Mbugwe "Umuhimu wa Kusoma kwa Bidii kuwaambia kwamba Dr. Samia Suluhu Hassan Ameendelea kutengeneza Mazingira Rafiki ya kufundishia na Kujifunza.Kisha amefanya mkutano wa hadhara kata ya Kisangaji.

 

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments