DRC WAASI WA M23 WAUZINGIRA MJI WA SAKE.

                           

Jeshi la Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Kongo limetumia ndege za kivita kuwarudisha nyuma waasi wa M23 waliokuwa wameuzingira mji wa Sake uliopo kilometa 27 magharibi mwa mji wa Goma jimboni Kivu Kaskazini.

Taarifa zinasema kuwa watu wasiopungua 7 walijeruhiwa  ndani ya kambi moja ya wakimbizi katikati mwa mji huo ambako hali ya wasiwasi ilitanda hadi Jumatatu jioni.

Mamia ya Watu  waliokuwa wameanza kurudi majumbani mwao mwishoni mwa wiki iliyopita waliuacha tena mji huo wa Sake baada ya wapiganaji wa M23 kuuzingira.

Vyanzo vya ndani vimeeleza kuwa kundi hilo linalodaiwa kupata usaidizi wa jeshi la Rwanda lilizidisha mashambulizi yake kwenye vijiji vya Kihuli, Kimoka na Luhonga kilometa karibu 5 na mji huo ambako milio ya silaha nzito iliendelea kusikika hadi jana jioni.

Akizungumza na wananchi wa Sake mwanzoni mwa juma hili Peter Chirimwami, gavana wa jijeshi mkoani Kivu Kaskazini alisema,

“Ikiwapo nimewasili hapa ni kwa ajili ya kuwatolea pole, juweni kwamba raisi anawawekea matumaini kuhusu Mnusco inabidi kuwa watulivu sababu mkiwashambulia mtampatia adui ushindi. Kamwe hatuta kubali mufanye fujo dhidi ya Monusco," alisema Chirimwami.

Mapigano hayo yanayoanza kuukaribia mji wa Goma yamesababisha watu zaidi ya milioni saba kuwa wakimbizi baadhi ikiwa ni wale kutoka wilayani Masisi na Rutshuru wanaohangaika sasa kwenye kambi za wakimbizi. 

Ripoti mpya  ya Umoja wa Mataifa, imeonesha kuwa jeshi la Rwanda linalounga mkono waasi wa M23 linatumia silaha  zenye uwezo wa juu kama vile makombora ya kutoka ardhini kwa kuzidungua ndege za kivita, vifaa vinavyoweza kuwapa uwezo wa kusonga mbele katika vita mashariki mwa Kongo.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments