Mwenyekiti wa chama cha soka mkoa Singida SIREFA mkoa Singida Hamisi Kitila akifafanua jambo katika mukutano mkuu wa kikatiba kwa kila mwaka.
Wajumbe wa mkutano mkuu wa SIREFA kutoka wilaya za Iramba,Manyoni,Singid dc,Singida mc,Supatanza,Flat,n.k na wadau mbalimbali katika mkutano huo.
wakati wa majadiliano juu ya maendeleo ya soka la vijana.
wakati wa majadiliano juu ya maendeleo ya soka la vijana.
Chama cha soka mkoa wa Singida Sirefa kimejipanga kuendeleza soka hasa la vijana katika mwaka mpya wa 2024 hiyo nikutokana na mwaka uliyopita wa 2023 kufanya vyema kwa akademi mbalimbali mkoani hapa.
Akitoa taarifa za michezo mbalimbali ambayo imefanyika kwa mwaka 2023 katika mkutano mkuu wa kikanuni wa kila mwaka mwenyekiti wa chama cha soka mkoa wa singida Hamisi kitila amesema kuwa msingi wa mpira wa miguu ni soka la vijana ambapo shirikisho la soka nchini TFF limekuwa likiandaa mashidano mbalimabali ya U15, U17 na U20 kwa lengo la kuandaa wachezaji wa baadae wa timu za soka kwa wanawake na wanaume pia.
0 Comments