WAZAZI WATAKAO KAIDI AGIZO LA SERIKALI MKOANI SINGIDA KUKIONA .

                                         

                                              Mkuu wa Mkoa akiongea na wakazi wa kijiji cha Kizonzo.


Mkazi wa kkijiji cha Mgela akiuliza swali kwa mkuu wa Mkoa katika Mkutano uliyofanyika katika kijii cha Mgale wilayani Iramba.


Mkuu wa mkoa wa Singida Pete Serukamba akitoatoa ufafanuzi wa matumizi bora ya matumizi ya Mbolea kwenye Mkutanao katika kijiji cha Mgale.

 

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Iramba Enosent Msengi akitoufafanuzi kwa Mkuu wa  Singida


         Mkuu wa mkoa Peter Serukamba akitoa ufafanuzi juu ya Ujenzi wa Zahanati ya kijiji cha Mukulu.

.


Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amewataka wazazi Wilayani Iramba Kuhakikisha wanawapeleka Watoto wao  Shule kwani ni agizo lililo tolewa na  Serikali nchini kuwa watoto wote walifaulu kujiunga na kidato cha kwanza wanarripoti Shule walizopangiwa ,

Serukamba alitoa Kauli hiyo  katika ziara yake ya kukagua Miradi mbalimbali ya Maendeleo katika vijiji vya Kisonga, Mkulu, Mgongo, Mseko, Kizozo, Mgela na Mtoa  Wilayani Iramba.

Akiwa  katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa alifafanya mikutano ya hadhara na kuongea na wananchi  wa vijji vya Kizonzo na Mtoa kusikiliza kero zao na kuzitolea ufafanuzi.

Serukamba ametoa wito kwa viongozi wote kuanzia ngazi ya Kata na Wilaya zote Mkoani Singida kuhakikisha wanafuatilia na kuhakikisha wanafunzi wote wa shule za Msingi na Sekondari wenye sifa wanaanza masomo .

Aidha Mkuu wa Mkoa alisema kuwa Mzazi yoyote atakaye shindwa kumpeleka mtoto wake shule atachukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kukamatwas na kufikishwa katika vyombo vya kisheria.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments