MATUKIO SIKU YA FAMILIA YA POLISI MKOANI SINGIDA

 

Mgeni Rasimi Mosese Machali Mkuu wa Mkalama.akitoa hotuba katika Siku ya Familia ya Polisi mjini Singida


                                             Mgeni Rasimi akiwa kwenye gwaride maalum


Utoaji wa vyeti kwaniaba ya waliofanya vyema kiutendaji kazi kutoka wilaya zote.


                                               zawadi kwa washindi wa mchezo wa mpira wa pete

                                                        

                                                           Uchangiaji damu pia ulikuwepo katika Bonanza hilo.


Mkuu wa Wilaya ya Mkalama MOSSES MACHALI amewataka wenza  wa Askari wa Jeshi la Polisi kuendelea kuwatia moyo askali hao ili wapate kuwa na utulivu wa akili ili waweze kutimiza majukumu yao kwa ufasaha na weledi.

 Machali alisema hayo  kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba wakati akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Familia ya  Kipolisi iliyofanyika mkoani Singida.

Alisema kuwa endapo familia za askaripolisi hazitakuwa nautulivu ni rahisi kwa askari kushindwa kutimiza majukumuyao kwa weldi kutokana na kukosa utulivu.

Naye Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida ACP Stella Mutabihirwa amesema kuwa lengo la Siku ya Familia ya Kipolisi ni kuimarisha ushikiano na kujenga umoja baina ya askari na familia zao na jamii kwa ujumla.  

Mutabihirwa aliongeza kuwa maadhimishi hayo huwakutanisha Polisi  ili  kupeana moyo kutokana na majukumu waliyonayo  ya kulinda usalam wa raia na mali zao.

Hata hivyo Mutabihirwa amewataka wanchi wa mkoa wa singida kuendelea kushirikiana na jeshi la polisi kufichua vitendo vya uhalifu na uvunjivu wa amnai kwa kutoa taarifa kila wakati.

Maadhimisho hayo yaliambatana na kufanyika kwa bonanza la michezo Mbalimabali ikiwemo  mpira wa miguu, mpira wa pete, riadha, Kufukuza kuku na Burudani mbalimbali.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments