MKOA WA SINGIDA UMEJIPANGA KUUNGA MKONO WAWEKEZAJI WA NDANI

 

Mkuu wa Mkoa Peter Serukamba akiongea na Mkurugenzi mkuu wa Kiwanda cha kusindika Mafuta ya Alizeti Khalidi Ally (kulia )

Mkuu wa Mkoa akioneshwa baadhi ya maeneo ya kiwanda hicho cha Mfuta ya Alizeti Mjini Singida,


                            Mkuu wa Mkoa Akiendelea na ukaguzi wa maeneo muhimu nadani ya kiwanda hicho.


                                             Mkuu wa Mkoa akipata maelezo katika ghala la Mshudu.

Khalid Ally akitoa shukrani zake kwa Mkuu wa Mkoa baada ya kumaliza ziara yake fupi huku akiipongeza Serikali kwa kuwajali wanachi wake hasa wakulima.


Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amesema kuwa serikali  mkoani humo  imejipanga kuhakikisha unaunga mkono wawekezaji wa ndani ya mkoa huo kwa lengo la kutengeneza ajira na fursa kwa wazawa na maendeleo ya Mkoa huo.

 Serukamba alitoa kauli hiyo katika ziara yake alipotembelea Ujenzi wa kiwanda cha usindikaji Alizeti cha Wild FLOWER Grant & Oil Mills Company Limited  kilichopo Manispaa ya Singida.

Alisema kuwa serikali ya Mkoa inaunga mkono uwekezaji huo kutokana na Rais wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kuendelea kuleta  Mbolea ya Ruzuku ili zao hilo liweze kuzalishwa zaidi Mkoani hapa kutoka na zao hilo kuwa ndiyo zao kuu la Biashara.

SERUKAMBA alisema kuwa tunataka kuona mkoa wa Singida unaingia kwenye Ramani ya taiafa katika uzalishaji wa Mfuta ya Alizeti na Mashudu ili kuongeza kipato cha Mkoa na Serikali kupunguza uagizaji wa Mafuta ya kupikia kutoka nje.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Wild Flower Grant & Oil Mill Company Limited Khalid Ommary Ally akiongea na Mkuu wa Mkoa alisema kuwa kiwanda hicho  kitaghalimu zaidi ya Dola  Mil 24 sawa na zaidi ya Bil 60 za kitanzania hadi kukamilika  kwake.

Khalid alisema kuwa Ujenzi wa Mradi huo unatarajia kukamilika mwezi Desemba Mwaka huu na  kuzalisha zaidi ya Lita 75,000 za Mafuta ya Alizeti kwa Siku, pamoja na kuajiri zaidi ya wafanyakazi 400,hadi 500 na kipaumbele kikiwa ni wakazi wa Singida.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments