BILIONI 3 KUTUMIKA UJENZI JENGO LA OFISI YA MANISPAA SINGIDA.



                   Jengo la Utawala la Ofisi ya Manispaa ya Singida linalo jengwa Mwenge mjini Singida.

                           

Mkuu wa Mkoa akipewa taarifa ya ujenzi wa jengo hilo na Mhandisi mbelea ya viongozi mbalimabali wa Wilaya akiwemo katibu tawala wilaya na Meya wa Manispaa.


Mkuu wa Mkoa Peter Serukamba(katikati)akikagua eneo la mradi katika Hospitali ya Manispaa baada ya kupata maelezo. 


Mkuu wa mkoa akipata maelezo mafupi kutoka kwa Mganga mkuu (DMO) wa Hospitali ya Manispaa Dr Anur Milulu baada ya kuoneshwa eneo linalotarajiwa kujengwa kwa fedha za Serikali.


Zaidi ya shilini bil 3 zitatumika katika ujenzi wa jengo la Utawala la Ofisi ya Halmashauri ya Manispaa ya Singida ikiwa ni fedha zilizotolewa na serikali.

Akisoma taarifa ya Mradi huo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Singida alipotembelea Miradi ya Maendeleo ya Manispaa ya Singida kaimu Mhandisi kutoka Ofisi ya Manisapaa  Karisto Mligo amesema kuwa ujenzi wa Mradi huo  mpaka sasa umeshatumia zaidi ya Mil 878 likiwa katika hatua ya ghorofa ya pili.

Naye Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Manispaa Singida Jeshi Lupembe alisema kuwa kwa sasa vifaa vya kukamilisha ujenzi huo vimesha nunuliwa mpaka sasa tunasubiri ni mfumo wa malipo ya fedha  ili tuweze kuendelea na ujenzi na kulipa fedha za mkandarasi zaidi ya sh Mil 51.l

Aidha Mkuu wa mkoa wa Singida Petert Serukamba akiongea baada ya kukagua jengo hilo ameutaka uongozi wa Manispaa kuhakikisha wanakamilisha jengo hilo kwa wakati, huku akiagiza halmashari  zote Mkoani Singida kutumia wakandarasi wenye uwezo ili kukamisha miradi kwa wakati .

Mkuu wa Mkoa Peter serukamba kabla ya kutembelea jengi hilo la utawala Manispaa ya Singida pia ametembelea Hospitali ya Manispaa ya Singida na kupata taarifa ya mwenendo wa Ujenzi na Ukarabati baada ya kupata fedha Tzs Mil 500 kutoka serikalini.

Akiowa katika Hospitali hiyo mkuu wa mkoa ameuwagiza uongozi wa Manispaa kuhakikisha vibali vya ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya Hospitali hiyo unaanza mara moja.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments