MAOFISA UGANI PIMENI AFYA YA UDONGO KWENYE MASHAMBA YA WANANCHI RC SERUKAMBA


Mkuu wa Mkoa Singida Peter Serukamba akiongea na wakuu wa idara mbalimbali wa halmashauri ya Itigi Wilayani Manyoni.


Madiwani wa Itigi wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Singida wakati akiongea na wakuu wa Idara juu ya usambazaji wa mbolea za ruzuku.



                                                          Watumishi wa Halmashauri.

Maofisa kilimo Mkoani Singida wameagizwa kupima afya ya ugongo kwenye mashamba ya wananchi na kuwashauri wakulima juu ya mazao yanayofaa kulimwa kulingana na afya ya shamba husika ili kulima kilimo chenye tija.

Akizungumza na viongozi wa halmashauri za Wilaya ya Manyoni na Itigi mkuu wa mkoa wa Singida Peter Serukamba amesema imefika wakati wa kuwapima viongozi kwa kutekeleza maagizo anayoyaagiza ili kuwanufaisha wakulima

Serukamba amesema hakuna namna nyingine ya kuongeza uzalishaji katika kilimo bila kutumia mbegu bora na matumizi sahihi ya mbolea za ruzuku zinazotolewa na serikali kwa lengo la kuwainua wakulima

Katika hatua nyingine Serukamba amesema viongozi wote wafanye kazi katika idara zao kwa weledi na kuacha tabia ya kuwabebesha wengine mzigo wa majukumu yote huku wengine wakikwepa wajibu wao.

Nao wataalamu wa kilimo wamesema elimu ya matumizi bora ya mbolea inaendelea kutokewa kwa wakulima ambapo idadi ya wakulima imeongezeka kwa msimu huu wa kilimo ikilinganishwa na msimu uliopita.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments