VIONGOZI WA HALMASHAURI ZOTE MKOANI SINGIDA HAKIKISHENI MBEGU ZENYE RUZUKU ZINASAMBAZWA.

 

                                      

                                            Mkuu wa mkoa wa Singida akiongea na viongozi kutoka wilayani.

Meya wa Manispaa ya Singida Yagi kiaratu akichangua juu ya usambazaji wa Mbegu unayoendelea katika eneo lake hasa pembezoni mwa mji wa Singida. 


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Itigi wilayani Manyoni Hussein Simba naye akitoa maoni yake sambamba na Ushauri kwa Serikali.


Ally Mwanga mwenyekiti wa Halmashauri ya Ikungi  akishauri jambo kwa mkuu wa mkoa.



Mwenyekiti wa Hlmashauri ya Wilaya ya Singida Dc Elia Digha akitoa wazo kwa mkuu wa mkoa nini kifanyeke juu ya usambazazi wa Mbegu hizo za Ruzuku.

                            

                               Wakirugenzi wa halmashauri ya Iramba na Manispaa ya Singida wakifuatilia hotuba.

                 Afisa Utumishi kutoka wilaya ya Singida Dc akitoa taarifa ya wilaya hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi.

Mkuu wa Mkoa wa Singida PETER SERUKAMBA amewataka Viongozi wa Halmashauri zote za Mkoa huo, kuhakikisha Mbegu za Alizeti zenye Ruzuku, zinasambazwa kwa wakulima.

Akiongea  katika Kikao kazi cha Mkuu wa Mkoa wa Singida, Viongozi wa Mkoa, Wilaya na Halmashauri zote Mkoa huu, kikao ambacho kilijadili Agenda mbalimbali za maendeleo ya Mkoa huo. 

SERUKAMA aliwataka Viongozi wa Halmashauri zote na Maafisa Ugani kutumia siku Sita (6) kuhakikisha Mbegu hizo sinasambazwa na kuwafikia wakulima katika Msimu huu wa Kilimo. 

Nao wajumbe wa Kikao Kazi hicho walisema ni vyema kuutumia Msimu huu wa Kilimo kubaini changamoto zilizojitokeza katika Misimu iliyopita ili kuzitatua kwa ajili ya misimu ijayo ya kilimo.

 Walisema endapo changamoto hizo zitatuliwa, na Begu zikawafikia wakulima kwa wakati itasaidia wakulima wengi kuzalisha kwa tija na kuongeza vipato vya familia zao na Taifa kwa ujumala.

 Hata hivyo baadhi ya wajumbe walisema bado kuna changamoto ya Bei kubwa ya MBegu ya Alizeti, hali inayosababisha wakulima wengi kushindwa kumudu Bei hizona kuenedelea kutumia mbegu za kienyeji.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments