KIPIMO CHENU NI UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YENU RC SERUKAMBA.

 


Mkuu wa Mkoa Singida Peter Serukamba akiongea na wakuu wa Idara mbalimabali wa Elimu na Maafisa Ughani wa halmashauri ya Itigi wilayani Manyoni.




Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Kemilembe Lwota amewaagiza kuandika barua ya maelezo kwa wale wahusika wa zoezi la uandikishaji wanafunzi katika hamashauri ya Itigi ilikujua chanzo cha kudolola katika maeneo yao.



Katibu tawala Mkoa wa Singida Dkt Fatma Mganga akisisitiza jamba huku akitoa maagizo ya utekelezaji wa majukumu yao.


Kikao kazi hicho cha utoaji taarifa mbalimbli za Elimu na usambazaji wa Mbolea pia kiliendelea halmashauri ya Manyoni Mjini



Mkuu wa Mkoa akitoa maelekezo kwa viongozi wa ngazi ya kata ya Kitaraka Itigi juu ya uandikishwaji wa wanafunzi


                                                Wataalamu na wakuu wa Idara Halmashauri ya Itigi.


                                

Wakuu wa Idara wa halmashauri ya Manyoni.
 

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amesema swala la watoto kwenda shule ni sheria ya nchi hivyo ni lazima viongozi na jamii kwa ujumla kuhakikisha watoto wote wanaopaswa kuanza shule ya awali, msingi na sekondari wanaenda shule.

Serukamba ameyasema hayo alipotembelea Wilaya ya Manyoni kata ya Kitaraka kuangalia zoezi la uandikishaji shuleni ili kuhakikisha kila mtoto anapata shaki ya msingi ya kupata elimu.

Amewaagiza viongozi kwenda kuwasaka watoto wote ambao hawajaandikishwa shule na kuanza taratibu za kuwachukulia hatua wazazi ambao wamewaficha watoto wao.

Aidha mkuu wa Wilaya ya Manyoni Kemilembe Lwota amesema ni jambo la fedheha kwa Wilaya hiyo kuwa wa mwisho katika zoezi la uandikishaji watoto shule na kuagiza viongozi wanaohusika na swala hilo kuandika barua na kueleza sababu za wao kutofuata maelekezo.

Hata hivyo mratibu elimu wa kata hiyo Cosmas Malamsha, afisa elimu Wilbert Chitanda na Mwenyekiti wa kijiji cha Dorotho wamesema changamoto kubwa ni baadhi ya vitongoji kuwa ndani ya mbuga ya Tanganyika Pakers ambapo miundombinu ya barabara sio rafiki hasa kwa kipindi hiki cha mvua na umbali mrefu wa shule ilipo.


Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments