FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO ZIPELEKWE KWENYE MAENEO HUSIKA RS SINGIDA.

 

                                   

                                    Mkuu wa Mkoa Singida Peter Serukamba akisisiza jambo katika kikao kazi.

  Katibu tawala wa Mkoa wa Singida Dkt Fatum Mganga akitoa maelekezo kwa wakuu wa wilaya na wakurugenzi.


 

                 Wakuu wa Wilaya wa Manyoni Kimilembe Lwota (kulia)na Thomas Apson wa Ikungi katika kikao hicho.

Kushoto ni Afisa Elimu Mkoa Dkt Baganda na Katibu tawala wilaya ya Singida Naima Chondo .


Wkuu wa Idara kutoka wilaya za mkoa wa Singida wakifuatilia na kupata maelekezo juu ya Miradi hiyo.


Zaidi ya Bil 5 zimepokelewa kutok Serikali kuu, kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya Miradi ya Maendeleo Mkoani Singida ikiwemo Madarasa na Umaliziaji wa Miradi ya Afya huku Miradi hiyo ikitakiwa kukamilika ndani ya Siku 90.

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe.Peter Joseph Serukamba,  amewaagiza   wakuu wa wilaya na wakurungenzi wote Wa halmashauri za Mkoa wa singida, kuhakikisha fedha zote za Miradi zinapelekwa mapema  kwenye maeneo ya Miradi.

Serukamba ametoa agizo hilo katika Kikao kazi Cha kupokea taarifa mbalimbali ikiwemo uandikishwaji wa wanafunzi shuleni, utekelezwaji wa Miradi ya maendeleo, usambazwaji wa mbegu na mbolea, na alitumia fursa hiyo kuwaagiza wakuu wa wilaya na wakurungenzi kuhakikisha fedha zote zilizotolewa na serikali  Kuu  zinafika mapema katika maeneo ya Miradi na ujenzi ufanyike kwa wakati.

Kwa upande wao wakuu wa wilaya za Ikungi na Manyoni, walisema wameyapokea maelekezo hayo kutoka kwa Mkuu wa Mkoa , na kukiri kuwa  kitendo Cha fedha hizo  kupelekwa katika maeneo ya Miradi itarahisisha kununuliwa mapema kwa vifaa vya ujenzi.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments