KITUO CHA TELEVISHEN CHA MGOMBEA URAIS DRC CHAPIGWA STOP.

 

                                                           Jenerali Maisa Ekenge

 Moja ya habari zilizozungumzwa sana tangu Krismasi nchini DR Congo ni pale ambapo jeshi la nchi hiyo liliposema kuwa limeiadhibu Televisheni ya Nyota na magazeti mengine kutokana na habari "kuvuruga, kuvunja moyo na kugawanya jeshi".

 

Katika taarifa yake, msemaji wa jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo alisoma kwa makini sana anachokisema, Jenerali Meja Sylvain Ekenge alisema kuwa siku za nyuma "Televisheni ya Nyota na magazeti mengine yanayofanya kazi kwa ajili ya adui yalieneza habari za uongo" kuhusu jeshi.

Anaongeza kuwa kwa sababu ya hili, jeshi linaweza "kuchukua hatua zinazohitajika ili kuhakikisha kwamba nguvu ya sheria inaheshimiwa."

Radio Okapi ya ONU na vyombo vingine vya habari vinasema kuwa Televisheni ya Nyota inamilikiwa na mgombea urais Moïse Katumbi ambaye anafanya kazi katika jimbo la Katanga.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments