ZAIDI YA BILIONI MOJA ZATUMIKA KUBORESHA SHULE KUPITIA MRADI WA SHULE BORA SINGIDA

 

Afisa Elimu Mkoa wa Singida Dkt Elipidius Baganda akifungua kikao kazi hicho.


Mratibu wa Mradi wa Shule Bora Mkoa wa Singida Fredrik Ndahani akiongea na wanahabari.



SINGIDA:

Kikao kazi cha mrejesho wa Mradi wa Shule Bora kimefanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida, kikilenga kujadili utekelezaji wa mradi huo, pamoja na kuangalia mafanikio na changamoto zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wake.

Mwenyekiti wa kikao hicho, Afisa Elimu Mkoa wa Singida Dkt. Elipidius Baganda, amesema kuwa mradi huo umeleta matokeo chanya kwa sekta ya elimu mkoani humo, ikiwa ni pamoja na kupatikana kwa zaidi ya shilingi bilioni moja kwa ajili ya ukarabati wa majengo, ujenzi wa shule mpya, na kuboresha miundombinu ya elimu.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Bi Anna Tutuba, pamoja na Afisa Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari wa wilaya hiyo Zipporah Simwanza, wamesisitiza kuwa programu ya Shule Bora imejipambanua kuhakikisha inaleta mabadiliko ya kweli. Wamewataka wakurugenzi wote wa halmashauri mkoani Singida kusimamia kwa makini fedha zinazotolewa ili kuhakikisha zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Naye Mratibu wa Shule Bora Mkoa wa Singida Fredrik Ndahani, amesema kikao hicho kimekuwa jukwaa muhimu la kutathmini utekelezaji wa mradi huo, kujadili mafanikio yaliyopatikana, pamoja na kutafuta suluhu za changamoto zilizojitokeza, hususan katika usimamizi wa fedha.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments