INADES FORMATION TANZANIA YAENDELEA KUTOA ELIMU KWA NJIA YA MASAFA NCHINI

 

SINGIDA


Mratibu wa Elimu kwa njia ya masafa Fortunata Tarimo kutoka shirika lisilo la kiserikali  la INADES FORMATINO TANZANIA kutoka Dodoma akitoa Elimu kwa wanavikundi vya Mkombozi na Huruma kotoka kijiji cha Kinyamwenda.


kazi ya ugawaji vitabau kwa wanavikundi ikiendelea.

wanakikundi cha Huruma wakiangalia vitabu hivyo baada ya kupatiwa ufafanuzi.


wanavikundi wakiendelea na usomaji wa vitabu hivyo.



Fortunata Limo akifafanua jambo kwa wanavikundi baada ya kuwapatia vitabu mbalimbali wanavikundi hao.

Katika kuahakikisha mwananchi, wakulima na wajasiliamali wanapata elimu na ujuzi mbalimbali katika kukuza uchumi shirika lisilo la serikali la maendeleo ya kiuchumi na kijamii  la INADES FORMATION TANZANIA limeanzisha mpango wa kutoa elimu kwa njia ya masafa.

Akiongea na standard radio Bi Fortunata Tarimo mratibu wa mafunzo kwa njia ya masafa amesema mafunzo hayo  yamegawanyika katika maeneo mbalimbali ikiwemo kilimo pamoja na uongozi na maendeleo

Bi,Fortunata ametaja baadhi ya vijitabu ambavyo wanavyo na vinatumika ilikutoa elimu kwa jamii.

Aidha Bi Fotunata amesema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuongeza ujuzi kwa jamii au vikundi mbalimbali nchini ili kuimarisha shughuli zake za kila siku na kuharakisha katika kuleta maendeleo.

Akizungumzia juu ya changamoto wanayokutana nayo katika utoaji elimu kwa njia ya masafa Bi Fortunata ameongeza kuwa ni namna bora ya usafirishaji kwa njia ya posta pamoja na baadhi ya maeneo mengine kutokuwepo na huduma ya posta na kuwafanya wadau kusafiri kutoka vijijini kuja mjini kufuata huduma hiyo ya posta wakati mwingine kusababisha upotevu wa vitabu nivyo.

 Elimu hiyo kwa njia ya masafaa nchini inatolewa katika mikoa mbalimbali nchini .


 

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments