Bi Catherine Kilongo Mfugaji wa kuku na Samaki akielezea na kuonesha aina ya kuu anaofuga.
Bi Sianeli Lyimo mfugaji wa Samaki akielezea manufaa ya ufugaji wa samaki kitaalamu.
SINGIDA
Wafugaji
kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Singida wameiomba serikali kuweka mkazo katika
kuwawezesha vijana waliomaliza masomo yao ili waweze kujiajiri kupitia shughuli
za ufugaji badala ya kusubiri ajira za ofisini.
Wito huo
umetolewa na Bi. Catherine Kilongo, mkazi wa Kijiji cha Mtinko, ambaye ni
mstaafu anayeendesha shughuli za ufugaji wa kuku na samaki. Bi. Kilongo amesema
kuwa baada ya kustaafu aliingia rasmi kwenye sekta ya ufugaji na amekuwa
akipata mafanikio makubwa ambayo aliwahi kuyakosa alipokuwa kwenye ajira ya
kawaida.
“Shughuli za
ufugaji zinalipa sana, kuliko hata ajira ya ofisini. Serikali iwasaidie vijana
kwa elimu na mitaji ili nao wajiajiri,” amesema Bi. Kilongo.
Kwa upande
wake, Bi. Sianeli Lyimo ambaye ni mfugaji wa samaki na aliyewahi kuwa muuguzi
(Nesi) katika kituo cha afya ndani ya halmashauri hiyo, amesema aliamua kuacha
kazi ya ajira rasmi baada ya kupata mafunzo ya ufugaji wa samaki. Kwa sasa,
anajitegemea kupitia mradi wake wa ufugaji na amekuwa mfano kwa vijana wengine.
“Vijana
wasisubiri ajira, waanze miradi yao. Ufugaji unalipa kama ukiamua kwa dhati,”
amesema Sianeli.
Wafugaji hao
wamesisitiza kuwa kwa mazingira ya Wilaya ya Singida, ambayo yanafaa kwa
shughuli za ufugaji wa aina mbalimbali, serikali ina wajibu wa kuongeza juhudi
katika kutoa mafunzo na mitaji kwa vijana ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi
na kupunguza tatizo la ajira
0 Comments