MWENGE WA UHURU WAANZA RASMI MBIO MKOANI SINGIDA

 

       

       Godwin Gondwen akitoa taarifa ya mbio za mwenge katika wilaya yake ya Singida Dc

            

         Mkuu wa Mkoa wa Singida akiongea katika mapokezi ya Mwenge katika kijiji cha Itaja 






Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Queen Sendiga akiongea wakati wa makabidhiano ya Mwenge.


                      

                   Wakuu wa Wilaya ya Singida wakiwa katika mapokezi ya Mwenge.

Singida

Mwenge wa Uhuru umeanza rasmi mbio zake katika mkoa wa Singida, baada ya kumaliza ziara ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika Mkoa wa Manyara.

Akizungumza mara baada ya kupokea Mwenge huo katika viwanja vya Kijiji cha Sagara, Kata ya Itaja, Wilaya ya Singida, Mkuu wa Wilaya ya Singida, Mheshimiwa Godwin Gondwe, alisema kuwa mkoa huo umejiandaa kikamilifu kuhakikisha Mwenge wa Uhuru unatembelea miradi ya maendeleo kwa mafanikio.

"Singida tumejipanga kuhakikisha Mwenge wa Uhuru unakimbizwa kwa usalama, huku ukikagua miradi ambayo ina tija kwa wananchi wetu."

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mheshimiwa Queen Sendiga, akitoa taarifa ya Mwenge wa Uhuru katika mkoa wake, alisema kuwa Mwenge huo umetembelea miradi 51 yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 71.3.

"Tumefanikisha ukaguzi wa miradi 51, na tunaamini utekelezaji wake utaendelea kuleta maendeleo endelevu kwa wananchi wa Manyara."

Naye, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ismail Ussi, amepongeza uongozi wa mkoa wa Manyara kwa usimamizi madhubuti wa miradi ya maendeleo, akiutaja kuwa ni mfano wa kuigwa.

"Hongereni Manyara kwa kazi nzuri. Miradi yenu inaonyesha matumizi mazuri ya rasilimali na dhamira ya kweli ya maendeleo."

Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kutembelea miradi 52 katika mkoa wa Singida yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 62, ukiwa na ujumbe wa kuhamasisha maendeleo, mapambano dhidi ya rushwa, magonjwa, na kushiriki uchaguzi kwa amani na utulivu.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments