HALMASHAURI KUTOA BIMA YA AFYA KWA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU

 

                               Robby Muhochi Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Ikungi.


                                

                             Mwl Donard Adam Mwalimu wa Shule ya Msingi ya Ikungi.

IKUNGI:

Na Mwandishi wetu.

Afisa Ustawi: Wazazi Hawana Uelewa wa Kutosha Kuhusu Malezi ya Watoto Wenye Ulemavu

Mwalimu Mlemavu Aeleza Changamoto za Kufundisha Wanafunzi Maalum Ikungi

Wazazi wengi wenye watoto wenye ulemavu bado hawana uelewa wa kutosha kuhusu malezi sahihi ya watoto hao, hali inayochangia changamoto katika ukuaji na maendeleo yao.

Kauli hiyo imetolewa na Afisa Ustawi wa Jamii wa Wilaya ya Ikungi, Bi. Robby Muhochi, wakati wa mahojiano maalum na kipindi hiki, kilipotembelea Shule ya Msingi Ikungi, shule ambayo hutoa elimu kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum pamoja na wasio na ulemavu.

Bi. Muhochi amesema kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi imejipanga kuwapatia wanafunzi zaidi ya 30 wenye mahitaji maalum huduma ya bima ya afya, kutokana na uhitaji wao wa huduma za kiafya mara kwa mara.

"Wanafunzi hawa wanahitaji uangalizi wa karibu kiafya, hivyo tumeona umuhimu wa kuwapatia bima ya afya ili kurahisisha upatikanaji wa matibabu."

Kwa upande wake, Mwalimu Donard Adam, ambaye ni mwalimu mwenye ulemavu anayefundisha katika shule hiyo, amesema changamoto kubwa wanayokabiliana nayo ni ukosefu wa vifaa vya kufundishia, hususan kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum.

"Tunayo changamoto kubwa ya vifaa maalum vya kufundishia, ambavyo ni muhimu sana kwa wanafunzi wetu ili waweze kujifunza kwa ufanisi."

Mwalimu Donard ameongeza kuwa kuwepo kwa vifaa hivyo kutasaidia wanafunzi hao kupata elimu bora na yenye usawa kama ilivyo kwa wengine.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments