RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN, AWAPA POLE MAJERUHI WA AJALI YA KUPOROMOKA KWA GHOROFA KARIAKOO

 





Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,Dkt Samia Suluhu Hassan akiwa katika Taasisi ya Tiba ya mifupa Muhimbili.


Dar -es-Salaam

Na Mwandishi wetu

Tarehe 20 Novemba, 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliwatembelea majeruhi wa ajali ya kuporomoka kwa jengo la ghorofa lililotokea Kariakoo, Jijini Dar es Salaam. Majeruhi hao wamelazwa katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI), Ilala.

Katika ziara hiyo, Rais Samia aliwajulia hali na kuwafariji waliopatwa na majeraha, huku akiwapa pole kwa msiba na changamoto waliokumbana nazo kutokana na ajali hiyo. Pia alitoa wito wa mshikamano na msaada wa haraka kwa wahanga wa tukio hilo, akisisitiza dhamira ya serikali katika kushughulikia majanga kama haya kwa ufanisi zaidi.

 

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments