MEXIME AWAOMBA WANA SINGIDA KUIUNGA MKONO TIMU YAO.

Kocha Mkuu wa Timu ya Ihefu Fc Mecky Mexime akiongea na wanahabari Baada ya mchezo wa Kombe la CRDB FERDERATION CUP kumalizika dhidi ya Mashujaa Fc na kupata ushindi kwa njia ya Mikwaju ya Penalti 


WAPENZI wa soka mkoani Singida wameombwa kutambua kuwa timu ya soka ya Ihefu,ni timu yao hivyo wanapaswa kuisapoti zaidi, ili iweze kuendelea kufanya vizuri kwenye ligi mbali mbali.

Wito huo umetolewa juzi na kocha mkuu wa Ihefu,Mecky Mexine muda mfupi baada ya kuitoa nje timu ya Mashujaa FC ya mkoani Kigoma, kwenye ligi ya kombe la CRDB Bank Federation .Kwa mikwaju ya penalty.

“Wana Singida hii Ihefu ni yenu wakiwemo na Wanyiramba. Msiiache kabisa kuisapoti kwa hali na mali.Ndugu zangu njooni….bila ninyi hatuwezi kabisa kwenda.Siogopi,mkiwepo na ari kwa wachezaji,inaongezeka zaidi”,amehimiza.

Amesisitiza zaidi kwamba mashindano hayo ni makumbwa (ni ya kimataifa),na yanaendelea bado… hatua moja mbele, yatahamia ngazi ya kimataifa.

Hata hivyo,mkongwe Maxime amewapongeza sana wapenzi wa soka waliojitokeza kuisapoti timu yao juzi, na kutoa sapoti iliyochangia Ihefu waweze kuwachapa wageni wao.

Dalili zilianza kuonyesha mapema kuwa Ihefu inaweza kuibuka na ushindi,baada ya kumiliki kipindi chote cha kwanza kwa kuliandama lango la wapinzani wao.

Hata hivyo wafungaji hawakuwa na utulivu pindi wanapolifikia lango la wenyeji wao.Wageni mashujaa wao walikimiliki kipindi cha pili mwishoni,na shida ni ile ile inafanana na ya Ihefu,umakini haukuwepo.

Kwa upande wake kocha mkuu wa Mashujaa,Abdala Mohammed,ametumia fursa hiyo kumshukru Mungu,kwa kumalizika salama mchezo huo ulikokuwa na ushindani mkubwa, hasa kipindi cha pili.

“Tumepoteza nafasi nyingi za kufunga hasa kipindi cha pili.Hali hii imechangia tuingie kwenye matuta ambayo kwa upande wetu,yametugharimu.Kwa ujumla hii ni ziara…..sasa tunafokasi kwenye ligi kuu”,amesema huku akionyesha wazi amesikitishwa na matokeo ya mchezo.

Mkazi wa tarafa ya Ihanja wilaya ya Ikungi,Isekuu Nathaniel,amemshauri Maxime mapema aangalie uwezekano wa kuipa jina jipya timu ya Ihefu (hili la Ihefu,halieleweki)Jina hilo jipya liwe na angalau harufu ya Kinyiramba,kinyaturu au hata la kisukuma wale wa wilaya ya Manyoni.

Amesema sio tu jina,viongozi waangalie uwezekano wa kuanzisha timu za viwango mbali mbali kila wilaya,ili kupata vijana wa mkoa huu, ambao watatangaza vema mkoa.

Tofauti na sasa ambapo timu zinaitwa majina ya Singida,lakini hakula hata mzawa mmoja ndani ya timu husika.Wote ni wa kuja na hivyo hawana kabisa mapezi ya kweli na mkoa wa Singida.

Katika hatua nyingine, meneja biashara wa  kanda ya kati,CRDB benki ,Andrew Mheziwa,alisema kuanzia sasa  wataanza kuhamasisha wananchi kupenda michezo ukiwemo wa soka kupitia CRDB.

“Kuanzia juzi tumeanza kutoa zaidi kwa mchezaji bora wa siku kwenye mchezo kati ya Ihefu na Mashujaa FC.Juzi tumemzawadi mchezaji bora Jeash Onyango wa Ihefu shilingi 500,000.Kiasi hicho cha fedha,kitapitia kwenye akaunti  ambayo itakuwa CRDB.Lengo tunataka kukuza michezo kupitia benki yetu”,amefafanua.

 

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments