DC MIRAJI MTATURU ATATUA MGOGORO WA MIAKA MINNE IKUNGU


     
MGOGORO wa Ardhi ya Shule ya Msingi Mnang’ana Kata ya Sepuka Wilaya ya Ikungi mkoani Singida uliodumu kwa miaka minne (4) kwa kushtakiana na mahakakamani kati ya viongozi na wananchi umemalizika juzi baada ya serikali kuamua kuyapima upya maeneo yote ya shule hiyo na sehemu inayobaki wananchi wakabidhiwe.

Habari za mwanzo kutoka shule hiyo zinasema kuwa watu watano walifikishwa Kituo cha Polisi Ikungi na mahakamani baada ya kudaiwa kuvamia maeneo ya shule kwa shughuli zao za kijamii isivyo halali na kukiuka maamuzi yaliyotolewa na Mkuu wa Wilaya ya Ikingi mwaka 2017 mwezi Julai baada ya kupewa ripoti kutoka kwa tume aliyoiunda.

Watu hao ni Yohana Maloda, Abdalaah Isango, Ramadhani Selemani, Saidi Selemani Sungi na Kijita Rajabu Mandi wanadaiwa kulima na kuchunga mifungo kwenye maeneo ya shule mwaka huu na wakashtakiwa kwa makosa ya kuvamia maeneo ya shule kinyume na amri ya serikali.

Katika mkutano wa hadhara juzi kijijini hapo maamuzi ya mgogoro huo Mkuu wa Wilaya ya  Ikungu  Miraji Mtaturu amesema Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Ikungi Mika Likapakapa alifika hapo kuangalia kati ya viongozi wa kijiji, uongozi wa shule na wananchi wana matatizo gani.

“Mtaturu amewataka viongozi wa serikali za vijiji kuwatumia wazee inapotokea matatizo kama haya kwenye maeneo yao ya migogoro ya ardhi ndipo maamuzi mengine yafanyike na hii itasaidia kwa kiasi kikubwa kuondoa ugomvi kati ya viongozi wenyewe na wananchi” Alisema.

Taarifa aliyoipewa Mkuu wa Wilaya na Afisa Ardhi juu ya mipango ya shule ina ekari 94.6 lakini kijiji kiliambiwa maeneo ya shule ni ekari 66 hapo mgogoro ukaanza ikabidi serikali kuyapima upya maeneo ya shule ili kujiridhisha.
Mtaturu aliendelea kusema maamuzi ya serikali kwa nia moja maeneo yote ya shule yalindwe, yaheshimiwe na yasivamiwe na watu ovyo ovyo yaachwe wazi kwa matumizi ya shule tu, hivyo mahusiano yaliyoharibika kijijini yarejee upya watu wasonge mbele katika kujiletea maendeleo.

Mtaturu amedokeza kuwa matatizo ya kijiji hicho siyo maeneo ya shule na mipaka yake ni mali yao bali ni chuki binafsi kwani shule ilipanda miti 137 na mikorosho 50 ikang’olewa  yote shule na serikali iliotoa miti hiyo ikapata hasara sasa waliyoing’oa wanaugomvi na serikali au wanaugpmvi na viongozi wa shule. Aliuliza.

Miti hiyo ilitolewa na serikali kwa gharama kubwa na ikapewa shule nayo tangu mwaka 2015 shule ingeanza kupata mapato siyo sahihi kung’oa miti akatoa mfano, “unapogombana na mwenye nyumba mbwa wake unampigia nini?”
“Sisi sote tukubali kulitokea makosa tangu mwanzo juu ya mipaka ya shule hii lakini sasa serikali imeliona hilo na serikali itapima upya eneo lote la shule zipatikane ekari 50 zinatosha kwa majengo yote ya shule yaliyobaki na zinazobaki viongozi wa serikali ya kijiji na wananchi watakaa, wataamua watazitumiaje.

Aidha Mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo Hamisi Abdalaah Mwangu amesema serikali katika kutatua mgogoro huo ilimtuma Afisa Ardhi kuweka bikoni kama alama ya mipaka ya shule na iliwekwa lakini baadhi ya wananchi wa kijiji hicho hawakukubali wa kuondoa moja wakavamia maeneo ya shule wakalima na kuchungisha mifugo.

Mwanga amesema hapo uongozi ukaanza kati ya uongozi wa shule na wananchi hao na viongozi wa kijiji wakafuata maagizo ya serikali mgogoro mkali ukaibuka ukafikia hatua mbaya mpaka kuchafua viongozi, viongozi wakawa wanalala na viatu wakihofia maisha yao lakini sasa maamuzi yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa Mtaturu yameleta amani kwa watu wote kijijini.

Naye kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Isack Mtinda amesema mgogoro wa shule yake sasa umeisha na kazi waliyonayo sasa ni kuchapa kazi, waliyopewa na taifa ili watoto wa wazazi wa kijiji cha mnang’ana wapate elimu.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments