ZOEZI LA KUKIJANISHA SINGIDA LAMALIZIKA SALAMA WILAYA YA MKALAMA (MATUKIO KATIKA PICHA



Mkuu wa wilaya ya Mkalama Mhandisi Jackson Masaka akifafanua jambo wakati akiongea na wananchi wa kijiji cha Yurason wilayani Mkalama wakati wa upandaji miti, ni katika zoezi la upandaji miti linaloratibiwa na Standard Fm 90.1 ya Singida huku zoezi hilo awali lilizinduliwa na Mkuu wa mkoa wa Singida Dr Rehema Nchimbi na kuanzia wilaya ya Ikungi,Iramba na sasa ilimemalizika Mkalama kabla ya kwenda wilaya ya Singida.,

wananchi wakipata maelekezo kabla ya kuanza upandaji wa miti hiyo.


Mkuu wa wilaya ya Mkalama Mhandisi Jackson Masaka akipanda mti.


Mwakirishi wa mkurugenzi wa Standard Fm Ally Juma akipanda mti.


Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Mkalama Mhandisi Godfrey Sanga akipanda mti.

Mshauri wa Jeshi la Mgambo wilya ya Mkalama akipanda mche wa mti.

Waandishi wa habari wa Teddy Mande na Revocatus Phinia wakijadili jambo wakati zoezi hilo la upandaji miti likiendelea.
Kaimu OCD wa wilaya ya Mkalama akionyesha namna ya kupanda mti.








Mwandishi wa Habari na Mtangazaji wa Standard Fm Teddy Mande akishiriki kikamilifu katika upandaji miti.


Festo Sanga mwandishi wa habari wa Standard FM akipanda mche  wa mti.








Mkuu wa wilaya ya mkalama mkoan Singida mhandis Jackson Masaka ameipongeza standard redio kwa kuanzisha kampen ya kuufanya mkoa wa singida kuwa wa kijani kwa kupanda miti.

Mhadis Masaka amesema hayo akiwa ofisini kwake wakati akitoa taarifa fupi juu ya upandaji miti katika wilaya yake kabla ya kuanza rasmi zoezi la kupanda miti katika kijiji cha Yulanson.

Masaka amesema kampeni hiyo ya upandaji miti itasaidia sana kuufanya mkoa wa Singida kuwamfano wa kuigwa katika maeneo mbalimbali.

Amesema jitihada mbalimbali za wadau zinahitajika iliuweza kupanda miti ya kutosha kwalengo la kuondoa hali ya ujangwa.

Ameiomba standard redio kuendeleza kampeni hii kwani inaendana na kampeni ya makamu wa rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania mama Samia Suluhu Hassan ya kuifanya Dodoma ya kijani.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments