MRADI wa kunusuru kaya maskini
nchini TASAF wilayani Ikungi umeweka mpango mkakati kuhakikisha kaya maskini
zinafikia hatua kubwa kiuchumi kwa kuwashirikisha walengwa ujenzi wa bwawa na
barabara ndogo vijijini na kazi zingine ndogondogo muhimu kwenye maeneo yao
kulingana na maelekezo ya viongozi wao.
Katika kuitikia wito huo kikundi
cha watu 133 na viongozi wao walioandikishwa kwenye mradi wa TASAF ya nguvu
kazi Kijiji cha Msungua Kata ya Sepuka wilayani Ikungi Mkoa wa Singida
wamejenga bwawa kubwa la kufugia samaki na kunwesha mifugo yao wakati wa
kiangazi na wametengebeza barabara km 6. Inayounganisha vijiji kwa nguvu zao
kwa siku tisini.
Wanatasafu hao wamepongezana kwa
kufanya sherehe ndogo baada ya kukamilisha kazi walizopewa utengenezaji wa
barabara km6 na bwawa baada ya kuchoshwa na ukosefu wa usafiri na usafirishaji
wa mazao yao kwenye soko kuu mjini Singida kwa mauzo.
Katika barabara hiyo kulikuwepo
na vichaka, magogo, vigogo, maji na tope hasa vipindi vya masika wanafunzi hao
walikuwa wanapata taabu kuvuka, mbuga yenye maji na tope kwenda shuleni katika
hali hiyo wanatasaf waliamua waitengeneze barabara hiyo ya kilomita 6 kutoka
ofisi ya Kijiji hadi Nyeghee kwa kwa kuondoa vichaka, magogo na maji pamoja na
kuipanua ili magari mawili yapishane.
Barabara hiyo itahamisha wananchi
inamopita barabara hiyo kulima mazao mikakati katika kujiletea maendeleo na wao
kupata usafiri na wanafunzi kufika shuleni bila kuchelewa na sasa wanaimba
Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi wafanye utaratibu barabara hiyo sasa iwape
TARURA wasaidie ujenzi wake.
Diwani wa kata ya Sepuka Halima
Ng’imba amewapongeza wanatasafu wa Kijiji cha Msungua kwa hatua walioifikia na
hiyo ndiyo dira ya Chama cha Mapinduzi wananchi kwenda na kasi anayotaka Rais
wao amewataka wanatasaf hao watakapopata malipo yao ya siku tisini wayatumie
vizuri yalete mafanikio kwao na kwa jamii.
Halima amesema barabara hiyo
inaunganisha vijiji vitatu Msungua, Irisya na Uhamaka na itarahisisha
usafirishaji wa mazao ya kilimo, mifugo na wao wenyewe kupata usafiri na
wanafunzi kupata urahisi wa kwenda shuleni bila woga pia akina mama wajawazito
na Watoto kusafiri hadi vituo vya huduma za kiafya kupata chanjo na tiba.
Kaimu Mratibu wa TASAF wilaya ya Ikungi
James Masolwa amesema Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi inawapongeza sana
wananchi wa Kijiji cha Msungua kwa kuonyesha maendeleo mazuri kwa ujenzi wa
bwawa na barabara itakayowaletea maendeleo.
Msolwa amesema maana ya serikali
ya Mama Samia kuanzisha mfuko huo wa TASAF ni kuokoa na kunusuru
kaya maskini nchini ili kuondokana na umaskini hivyo walengwa watumie fedha
watakazopata kusomesha Watoto wao na kuweka akiba na kupata huduma za msingi
kutokana na mfuko huo.
Aidha Afisa Mtendaji wa Kata ya
Sepuka Abella Kibanda amedokeza mradi huo ukiisha uache mafanikio Kata ya Sepuka
kwa kuwaletea wananchi maendeleo makubwa kwa kupunguza umaskini ndani ya jamii
na itakuwa vizuri kama barabara hiyo itaingizwa TARURA ili iweze kujengwa
vizuri ili itumike muda wote.
Baadhi ya wakazi wa Kijiji hicho
Abdallah Jingi, Elifuraha Ambarangu, Juma Hango, Missai Senge na Hassani
Megheko wamesema ni vema barabara hiyo iandikishwe TARURA, ipanuliwe vizuri
sehemu korofi ili wanakijiji wasafiri wao wenyewe na kusafirisha mazo
wanayolima.
Mwisho.




0 Comments