NAIBU meya manispaa ya Singida Mhe
Geoflya Mdama,amesema kuwa mkoa wa Singida utaendelea kusapoti michezo mbali
mbali, pamoja na mambo mengine,mkoa unaweze kutangazwa ndani na nje
ya nchi kupita michezo.
Naibu huyo ametoa kauli hiyo muda mfupi baada ya
kukagua timu ya Singida Black Star na timu kutoka Burundi ,Aigle
noir.Mchezo huo umefanyika uwanja wa Leti mjini Singida.
Ili kufikia lengo amewataka vijana wajitokeza kwa
uwingi kuonyesha vipaji vyao,waweze kuendelezwa kwa faida yao na
mkoa kwa ujumla.
“Tunatarajia mbele ya safari,mkoa wetu
utakuwa umetangazwa zaidi pengine zaidi ya Yanga na Simba za
Dar-es-salaamu”,Mdama amesisitiza ambaye alimwakilisha meya wa
manispaa ya Singida Yagi Kiaratu.
Katika hatua nyingine,timu ya Singida Black star,iliichapa
Aigle noir ya Burudi, goli moja kwa bila.Goli hilo lilifungwa na Joseph Guede
katika dakika ya 72 kipindi cha pili.
Hata hivyo,viongozi wa maandalizi ya hafla hiyo
iliyotumika Singida Blach Star kutangaza wachezaji wake pamoja na benchi la
ufundi likongozwa na kocha mkuu Patick Ausseams,walifuta viingilio hivyo, na
wapenzi kuingia bure kuangalia mchezo huo.
Ni jukwaa kuu, ndilo lilijaza wapenzi
wengi wa soka,huku jukwaa la mzunguko,likiwa na watazamaji wachache
mno.
Ayubu Yangu wa Singida Black Star amewapa matumaini
wakazi wa mkoa wa Singida,kwamba waondoe hofu timu inaenda kufanya vizuri
kwenye michezo ya ligi kuu, inayotarajiwa kuanza agosti 18 mwaka huu.
Singida itaanza kucheza na timu ya
Mbeya city ambayo mchezo huo utafanyika jijini
Mbeya agosti 18 mwaka huu.Wapenzi wa soka mkoa wa Singida,watarajie
pointi tatu.
0 Comments