Urusi inawahamisha wakaazi wake kutoka eneo la pili la mpaka, huku Ukraine ikiendelea na mashambulizi ya wiki moja ndani ya nchi hiyo.
Takriban watu 11,000 katika eneo la Belgorod wamehamishwa, vyombo vya habari vya serikali ya Urusi viliripoti, kwa sababu ya "hatua ya adui" karibu na mpaka.
Belgorod iko karibu na Kursk - ambapo wanajeshi wa Ukraine walianzisha shambulio lao la kushtukiza katika eneo la Urusi Jumanne iliyopita.
Vikosi vya Ukraine vimesonga mbele hadi maili 18 (km 30) ndani ya Urusi –ikiwa ni uvamizi mkubwa zaidi nchini humo tangu uvamizi kamili wa Moscow nchini Ukraine.
Kyiv inadai maelfu ya wanajeshi wanahusika.Siku ya Jumatatu asubuhi, wakaazi katika sehemu za Belgorod - ambayo iko kusini mwa Kursk - waliambiwa wasiwe na hofu lakini lazima wahame.
Gavana wa Belgorod Vyacheslav Gladkov alisema raia katika wilaya ya Krasnaya Yaruga walikuwa wakihamishwa kutokana na "shughuli za adui kwenye mpaka".
Pia alisema eneo lote lilikuwa chini ya tahadhari ya makombora, na aliwaambia watu wajifiche katika vyumba vyao vya chini.
Lakini aliongeza kuwa "ana uhakika kwamba wanajeshi wetu watafanya kila kitu kukabiliana na tishio ambalo limetokea".
Watu pia walikuwa wakiendelea kuhamishwa kutoka Kursk Jumatatu - na maelfu ya watu waliambiwa waondoke majumbani mwao katika wilaya ya Belovsky.
Gavana wa Belovsky Alexei Smirnov pia alitoa onyo la kombora - akisema watu walihitaji kujificha katika vyumba visivyo na madirisha na kuta thabiti.
0 Comments