Doha Qatar
Pongezi hizo zimetolewa hivi karibuni wakati Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na
Rushwa (TAKUKURU), Bw. Crispin Francis Chalamila alipotoa taarifa ya Tanzania
kuhusu utekelezaji wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa dhidi ya Rushwa kwenye
Mkutano Mkuu wa 11 wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Mataifa dhidi ya Rushwa
unaoendelea jijini Doha, Qatar. Mkurugenzi Mkuu Chalamila anaongoza ujumbe wa
Tanzania kwenye Mkutano Mkuu huo ulioanza tarehe 15 hadi 19 Desemba, 2025
jijini Doha, Qatar.
Akiwasilisha taarifa ya
utekelezaji wa Mkataba, Bw. Chalamila alisema “Rushwa inaendelea kuleta changamoto katika mataifa
mmbalimbali kwa kudhoofisha utawala, kudorora kwa ukuaji wa uchumi, kuongezeka
kwa umaskini, kukiukwaji wa haki za binadamu, huduma za umma zisizo na tija,
kudhoofisha taasisi na maendeleo potofu.”
Aidha, Tanzania
imepongezwa kwa kuimarisha mifumo ya uzuiaji rushwa kupitia utekelezaji wa
Mkakati wa Kitaifa dhidi na Rushwa na Mpango wa Utekelezaji (NACSAP IV),
kuboresha mifumo ya manunuzi ya Umma kupitia Sheria ya Ununuzi ya Umma ya mwaka
2023, kuimarisha utaratibu urejeshaji wa mali zilizpopatikana kwa njia za
uhalifu ikiwemo rushwa kupitia Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, na kuimarisha
taasisi simamizi ikiwemo TAKUKURU, Kitengo cha Kudhibiti Fedha Haramu, Ofisi ya
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na Sekretarieti
ya Maadili ya Viongozi wa Umma.
Alieleza kuwa, kufuatia
kukamilika kwa Mzunguko wa Mapitio ya Kwanza wa Tanzania Kupimwa ilivyotekeleza
Mkataba wa UNCAC (First Review Cycle), uliofanywa na nchi za Austria na
Msumbiji, Tanzania ilionekana kuwa imefanya mageuzi makubwa katika kuimarisha
mfumo wa kitaifa wa kudhibiti uhalifu, utekelezaji wa sheria na kuimarisha ushirikiano
wa kimataifa.
Mkutano Mkuu wa 11 wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Mataifa dhidi ya
Rushwa hufanyika kila baada ya miaka miwili ukiwakutanisha wakuu wa taasisi
simamizi dhidi ya rushwa, watunga sera, viongozi wa kisiasa, asasi za kiraia,
asasi zisizo za kiserikali, pamoja na wadau wa maendeleo. Mkutano huu
unaoendelea jijini Doha umekutanisha washiriki zaidi ya 3000 kutoka mataifa
mbalimbali chini kauli mbiu inayosema “Shaping Tomorrow’s Integrity.”





0 Comments