Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU Mkoa wa Singida imeokoa kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 28 kwenye miradi 5 yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 4 iliyokuwa ikitekelezwa mkoani humo.
Mkuu wa taasisi
hiyo Mkoa wa Singida Sipha Mwanjelwa ametoa taarifa hiyo wakati akizungumza na
waandishi wa habari kutoa taarifa ya utendaji kazi wa kipindi cha januari hadi
machi mwaka huu.
Amesema Kufuatia
ufuatiliaji uliofanywa na TAKUKURU kwa kipindi hicho miradi 5 ilikutwa ina
mapungufu ikiwemo kufanya malipo ya vifaa vya ujenzi kwa wazabuni yanayohusisha
gharama ya Kodi ya ongezeko la thamani (VAT) wakati wazabuni hao hawajasajiliwa
kwenye mfumo huo.
Hata hivyo Mkuu
huyo amesema kwa robo ya nne ya kuanzia mwezi aprili hadi juni mwaka huu
TAKUKURU imeweka mikakati ya utendaji kazi,huku akitoa rai kwa wananchi
kujiepusha na vitendo vya rushwa na kushiriki kikamilifu katika kuzuia vitendo
hivyo.









0 Comments