MKUU WA WILAYA YA SINGIDA ATOA ONYO KWA WAFANYABIASHARA WANAOKWEPA USHURU.

 SINGIDA.

Mkuu wa wilaya ya singida muhandisi Paskasmuragili amewatahadhalisha wafanya biashara wenye tabia ya kukwepa ushuru wa serikali kuwa waache mara moja, serikali ya wilaya ya Singida itaendelea kuhakikisha inafanyaa ukaguzi wa kila gari la mizigo  linalopita katika wilaya ya Singida na litakaguliwa kama lina nyaraka halali za kusafirishia mizigo hasa mazao.

Kauli hiyo ameitoa baada ya kukamata maroli matano ya shehena ya  mizigo ya maharagwe,pumba na mchele yaliyokuwa yakitokea mkoa wa Kagera (bukoba)  na kuelekea jiji la Arusha yakiwa hayana nyaraka halali za  malipo ya ushuru ya serikali Zaidi ya shiringi 4,900.000/= huku kukiwa na udanganyifu wa baadhi ya nyaraka.

Baada ya tukio hilo lililo tokea eneo la njia panda kati ya wilaya ya Singida DC na manispaa majira ya saa 12.00 asubui mkatisha ushuru Bw Juma Athumani hakuridhishwa na nyaraka za mizigo hiyo na kuamua kuyazuia magari hayo na kutoa taarifa kwa ungozi ambapo kamati ya ulinzi na usarama ya wilaya ilifika na kujionea ikiongozwa na mkuu wa wilaya ya Singida na kuamuru malipo halali ya ushuru wa serikali  yafanyike ndipo magari hayo yaendelee na safari..

katiki ni mkuu wa wilaya ya Singida Muhandisi paskas muragili akiongea na baadhi ya wamiliki wa magari hayo yenye shehena ya maharagwe na mchele katika eneo la tukio.







Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments