DR MAHENGE ANENA NA WATUMISHI WA MANISPAA YA SINGIDA.

 

Na. Yuzarsiif Labia : Singida.

Mkuu wa Mkoa hapa Singida, Dkt. Bilinith Satano Mahenge, ameanza ziara yake ya kukagua maeneo kadhaa yaliyochini ya halmashauri ya manispaa ambapo leo ametembelea jala (Dampo)  kubwa za taka ngumu, soko la vitunguu lililopo kata ya misuna na mradi wa kilimo cha umwagiliaji kisasida.

Dkt Mahenge amebaini changamoto zinazokabili maeneo hayo   na wananchi kwa ujumla ikiwa suala kubwa ni hali ya usafi wa mazingira kutoridhisha kisha kumuagiza Kaimu Mkurugenzi wa manispaa, Deus Luziga kuondosha taka ngumu zilizojaa katika Jala (Dampo) zote ndani ya siku tatu pamoja na kuweka utaratibu wa usafi wa kila siku katika maeneo hayo ili kuepusha hatari ya magojwa ya milipuko.

Akisisitiza katika hatua za kimaendeleo ili Singida kufikia kuwa jiji, Dkt Mahenge amesema ni lazima miundombinu ya barabara na sehemu zingeine kuimarishwa na akitolea mfano wa mtaa ya Sabasaba, barabara zinahitaji kufanyiwa marekebisho ndani ya wakati.

Hata hivyo ameonesha kutoridhishwa na mwenendo wa ukusanyaji wa mapato, katika halmashauri hapa singida na kusema kwamba‘matapo mengi yanapotea kutokana na kukosa usimamizi bora hali inayopelekea upotevu mapato ya serikali.’

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya hapa Singida Muhandisi Pascus Muragili akieleza kuhusu tatizo la usafi wa mazingira ambalo liliibua sitofahamu kwa Afsa mazingira Bi, Arafa Halifa, amesema manajimenti ya manispaa haina ushikiano mzuri baina yao katika kutatua kero za wananchi.

Aidha kuhusu suala la soko la vitunguu Msufini,Mkuu wa Mkoa, ametembelea na kujionea adha  zinazolikabili eneo hilo ,na mwenyekiti wa soko Iddi swalehe mwanja amesema licha ya kuwa na changamoto nyingi lakini wameendelea kupiga hatua nzuri, na kuomba kutatuliwa kero zinazochelesha maendeleo ya soko hilo.

Mkuu wa Mkoa Dkt. Bilinith Satano Mahenge ,anafanya ziara ya siku mbili ,katika kutembelea maeneo tofauti tofauti yaliyopo ndani za halmashauri ya manispaa ya Singida ili kujionea changamoto na shughuli mbalimbali zinazofanyiwa na wananchi  katika maeneo hayo hususani katika vyanzo vya mapato.

Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt Bilinith Mahenge akiongea na watumishi wa serikali kutoka idara mbalimbali katika manispaa ya Singida mjini Singida mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa RC mission huku baada ya mkutano huo alifanya ziara ya kutembelea maeneo mbalimbali ya manispaa ya Singida.


Kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya manispaa ya Singida na mchumi wa Halmashauri Bw Deusi Luziga akimkaribisha mkuu wa mkoa wa Singida katika kikao maalum.

mkuu wa wilaya ya Singida muhansi Paskas muragili akiongea kabla ya kumkaribisha mkuu wa mkoa wa Singida kuzungumza na watumishi na wakuu wa idara.


                              

watumishi wakimsikiliza  mkuu wa mkoa Dkt Mahenge.


kaimu mkurugenzi wa manispaa ya Singida akimkaribisha katika jengo la ofisi za manispaa ya Singida ikiwa ni mara ya kwanza kufika katika ofisi hizo.



Ni baada ya kuingia ndani ya jengo la ofisi za manispaa ya singida na kubaini uchakavu wa jengo hilo .

Mkuu wa mkoa akipata maelezo juu ya taka zilizozagaa katika moja ya guba la eneo la stendi ya zamanai kutoka kwa kaimu mkurugenzi wa manispaa.


baada ya kupata maelezo juu ya changamoto ya ukosefu wa gari la taka lililo alibika mkuu wa mkoa (Hayupo katika picha ) alifika katika gereji ya TEMESA kujionea hali ya gari hilo.
mkuu wa mkoa ametembelea soko la kimataifa la vitunguu lililopo katika kata ya Misuna na kuongea na uongozi wa soko hilo mwenye kanzu nyeupe ni mwenyekiti wa soko hilo Bw Mwanja akimtembeza mkuu wa mkoa wa singida wa kwanza kulia.
katikati ni mwenyekiti wa soko hilo akitoa maelezo mafupi juu ya hali ya biashara ya msimu wa vitunguu kwa mwaka huu.


pia mkuu wa mkoa alitembelea katika mradi wa kilimo cha umwagiliaji kilichopo katika kata ya Kisasida mjini hapa.


ni matenki makubwa ya kuhifadhiwa maji kwaajili ya kilimo hicho yaliyokaa kwa muda bila kutumika kutokana na ukosefu wa nishati ya umeme.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments