MAADHIMISHO YA SIKU YA MKULIMA SHAMBANI

Kutoka IKUNGI

Katika kuadhimisha siku ya mkulima shambani shirika lisilo la kiserikali la  UN WOMEN kwa kushirikiana na FARM AFRIKA  na kwa insani ya KOICA waliandaa hafla fupi iliyofanyika katika shamba darasa katika kijiji cha Mnang”ana kata ya Sepuka wilaya ya Ikungi mkoani Singida.

Akiongea katika hafla hiyo mgeni rasimi mkuu wa wilaya ya Ikungi Mhe Edward Mpogolo amefuraishwa na elimu iliyotolewa kwa Zaidi ya wakulima miatatu hamsini katika vikundi mbalimbali ikiwa ni ndani ya mwaka mmoja wa utekelezaji wa mradi huo wa kilimo cha Alizeti kupita mashamba darasa mbalimbali.

nimeaalifiwa kupitia taarifa niliyopewa kuwa fedha za mradi huu ni shiringi mili miatisa 900 lakini mpaka sasa ndani ya mwaka mmoja fedha zilizokwisha tumika ni Zaidi ya shili milioni miatatu na tisa katika mwaka mmoja nimefurai sana.

Bw Tumaini Elibariki ni program meneja wa mazao ya kilimo kutoka shirika la FARM AFRIKA alifafanua zaidi juu ya namna shirika hilo linavyo hakikisha elimu inayotolewa inakuwa na tija kwa wanawake wakulima wa zao la Alizeti katika wilaya ya Ikuingi, pia amesema kuwa lengo la mradi huu ni kuwezesha wanawake kiuchumi na kutetea usawa wa kijinsia sambamba na kuwapa elimu Zaidi juu ya kilimo cha Alizeti.

Bi Zainabu hamisi na Bw Ramadhani hamisi Kitifui ni wanufaika wa mradi huo wanaelezea nanmna walivyoweza kuitumia Elimu hio na kupata manufaa katika familia yao, "Tumenufaika sana na ujio wa shirika hili kwani wametupa elimu juu ya kilimo bora cha Alizeti mimi na mkewangu tayali tuna shamba darasa hili hapa unaona jinsi Alizeti ilivyostawi vizuri amesema mzee Ramadhani Kitiku".

 


Mkuu wa wilaya ya Ikungi Mhe,Edward Mpogolo akiongea na wananchi katika Hafla hiyo ya siku ya mkulima shambani.

Tumaini Elibariki ni Program Meneja wa shirika la Farm Afrika akitoa taarifa fupi ya mradi.

                                       
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi Bw Justice Kijazi akitoa neno la shukrani kwa wadau mbalimbali waliohusika katika zoezi zima la maandalizi ya shughuli hiyo.




mkuu wa wilaya na meza kuu wakitembelea mabanda mbalimbali ya wadau katika hafla hiyo.







Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments