CARLOS PUYOL APIGWA STOP IRAN


Beki wa zamani wa Barcelona na Uhispania Carles Puyol amepigwa marufuku kushiriki kipindi cha kombe la dunia nchini Iran kwa kuwa na nywele ndefu.

Licha ya kukubali kushiriki kwenye kipindi cha kutangaza mechi ya kombe la dunia kati ya Uhispania na Iran, na hata kuwasili Iran, Puyol alilazimika kusalia kwenye hoteli baada ya kunyimwa ruhusa kutangaza mchuano huo.

Puyol alitarajiwa kushirki kipindi hicho spesheli kwenye kituo cha IRTV 3 akiwa na mtangazaji Adel Ferdosipour.

"Namna mnavyojua, nilitarajiwa kuwa na Carles Puyol studioni leo, lakini yuko hotelini kwa sasa. Licha ya juhudi zangu zote, hatukufanikiwa. Tunaomba radhi,"Ferdosipour alisema.

Bwana Puyol alifahamishwa na idhaa ya taifa ya IRIB hangeweza kushiriki kwenye kipindi kwani nywele zake zilikuwa ndefu.
Idhaa ya taifa ya Iran haina sheria juu ya mtindo wa nywele lakini mambo yanayokinzana na mafunzo ya Kiislamu huzuiwa.
 
Aidha, sheria za shirikisho la soka la Iran zinawazuia
wachezaji dhidi ya kuwa na mtindo wa nywele
'unaoeneza
mitindo ya kigeni' na wachezaji huonywa dhidi ya kuwa
na
mitindo ya nywele inayokatazwa.
Hii sio mara ya kwanza hali kama hii kushuhudiwa kwenye runinga ya Iran.

Miaka miwili iliyopita, kipa wa timu ya taifa ya soka ya ufuo Peyman Hosseini, alizuiwa kushiriki kipindi cha televisheni kwa sababu ya nywele zake. Aidha, alikataa pia kuzifunika.

Uamuzi wa kumzuia Puyol unajiri wiki chache tu baada ya mkurugenzi wa IRTV3's Ali Asghar Pourmohammadi, kuondolewa na nafasi yake kupewa afisa mwenye misimamo mikali ya kidini.

Hata hivyo naibu mkuu wa idhaa ya taifa (IRIB), Morteza Mirbaqeri amenukuliwa Jumamosi akipinga madai hayo.

Shirika la Jam-e Jam daily linalomilikiwa na IRIB, limemtaja bwana Mirbaqeri akisema "Idhaa ya taifa inapinga madai hayo asilimia 100% ".

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments