UZINDUZI WA JUKWAA LA USHIRIKA MKOANI SINGIDA


Mkuu wa wilaya ya Singida Elias Tarimo 
MKUU wa Mkoa wa Singida,Dk.Rehema Nchimbi amewaagiza viongozi wa vyama vya ushirika kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ya ushirika kuanzisha viwanda vya kuongeza thamani ya mazao katika vyama vyao vya ushirika.

Dk.Nchimbi ametoa agizo hilo katika hotuba yake ya ufunguzi iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa wilaya ya Singida,Bwana Eliasi Tarimo kwenye uzinduzi wa jukwaa la wanaushirika Mkoa wa Singida lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kanisa Katoliki mjini Singida.

Aidha mkuu wa wilaya huyo hata hivyo ameweka bayana kwamba mkoa wa Singida ni maarufu kwa uzalishaji wa mazao mchanganyiko ikiwa ni pamoja na alzeti,mtama,pamba,mazao ya mifugo,lakini hakuna viwanda vya ushirika vilivyoanzishwa kwa ajili ya kusindika mazao hayo.

Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Mkoa ni wajibu wa viongozi na wanachama wenyewe kuhakikisha vyama vinatunza mitaji yao ya ndani kwa kuweka akiba mara kwa mara,kulipa hisa,kuweka amana naa kutenga mafungu ya lazima kutokana na faida na kutafuta vyanzo vingine vya fedha.

Akisoma taarifa ya Maendeleo ya ushirika ya Mkoa wa Singida kwa niaba ya Mrajisi msaidizi wa Mkoa,Afisa ushirika wa Halmashauri ya Itigi,Bwana Charles Martin Madula amefafanua kwamba ni ukweli kwamba ushirika wa mazao mchanganyiko yakiwemo mazao ya alzeti,ufuta,dengu,mbaazi na pamba umekuwa haufanyikazi ya kuwahudumia wanachama wake kwa kipindi cha kirefu sasa.


Kwa upande wake Mwakilishi wa vyama vinavyplima zao la tumbaku katika Halmashauri ya Itigi,Wilayani Manyoni,Bwana Martin Petro Mdemwa ameweka bayana kwamba vyama vya Idodomya Amcos,Manyanya Amcos,Isingiwe Amcos,Mtakuja Amcos na Umoja Amcos vinakabiliwa na changamoto ya soko la kuuzia kilo 58,770.14 za tumbaku.
Mwana ushirika wa ufugaji Nyuki na mshindi wa nane nane mwaka 2017  Bw Kiemi akitoa ushuuda wake katika ulinaji wa  asali.
mwanaushirika kutoka katika sekta ya madini akitoa ushuhuda wake pia.
Baadhi ya wanaushirika mkoa wa Singida wakipiga picha na mgeni rasimi.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments