MISOKOTO 7360 YA BANGI MBALONI SINGIDA


Kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Singida ACP Debora Magiligimba akionyesha  mihadarati hiyo ofisini kwake.

Kamada Mgailigimba akiwa katika ukaguzi wa magari barabara kuu ya Mwanza.


Mbwa wa Polisi akikagua basi la Mgamba kutoka Arusha kwenda Mwanza.



Jumla ya misokoto 7360 ya bangi imekamatwa na jeshi la polis mkoa wa Singida pamojana na kilo 41 na gramu 220 za milungi katika operesheni inayoendelea nchi nzima ya kupambana na madawa ya kulevya.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kamanda wa jeshi la polis mkoania Singida ACP Debora Magiligimba amesema oparesheni hiyo imeanza tarahe 1mwezi wa pili mwaka huu na kufanikiwa kukamata madawa ya kulevya ya aina mbalimbali

Kamanda Magiligimba amesema wanafanya ukaguzi wa mabasi yanayoingia mkoani hapa kwa kutumia mbwa ambao wamaepata mafunzo ya kubaini madawa hayo
Amesema watuhumiwa saba wamefikishwa mahakamani kwa kujihusisha na biashara hiyo huku watuhumiwa 13,wakisubiri majarada yao kukamilika kwa hati za mashtaka kutoka kwa mwanasheria wa kanda mkoa wa Singida.


Amesema zoezi hilo ni endelevu huku akiwaomba wananchi kutoa ushirikiano wa kutosha ili kuhakikisha wanatokomeza la madawa ya kulevya

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments