MBIO ZA UBINGWA BADO ZIPO PALEPALE SULEIMAN MATOLA.

 



Pamoja nakupoteza mchezo wa CRDB FEDERATION CUP bado benchi la ufundi  Mnyama Simba limejipanga kuhakikisha lina endeleza  mpango wake wa kutwaa ubingwa wa ligi kuu NBC PREMIER bara,Kuelekea mchezo baina ya wenyeji Ihefu fc Dhidi ya Mnyama Simba Sport Club unaotarajiwa kuchezwa Mjini Singida jumamosi ya April 13  CCM LITI STADIUM  viongozi wa mabenchi ya ufundi wamekutana na wanahabari katika ofisiu ya Bank ya NBC lililopo katikati ya Manispaa ya Singida.

Wakijibu maswali ya waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali katika kikao cha kikanuni ya ligi kuu NBC kocha msaidizi wa timu ya Simba Suleiman Matola amesema kuwa mchezo huo hautakuwa mwepesi kutokana na ubora wa usajiri wa timu ya Ihefu waliyoufanya katika dirisha dogo la usajiri la msimu huu.

Matola amewataka mashabiki wa Simba kujitokeza kwa wingi katika mchezo huo ili kuwapa moyo na morali wachezaji wao kwani wamejipanga kupata matokeo mazuri  kwani pointi tatu ni zamuhimu ,kwa upande  wake nahodha msaidi wa Simba Mohamed Hussein amesema kuwa tunajua mashabiki wamesikitishwa na matokeo yaliyopita lakini kwa mchezo huu tutahakikisha tunawafurahisha na kuwapa faraja.

Naye kocha mkuu wa timu ya Ihefu fc Mecky Mexime amesema kuwa Tunawaheshimu Simba kwani  ni timu kongwe  na bora nchini lakini tutahakikisha tunapata point tatu muhimu ikumbukwe kuwa kwa msimu huu tumejiwekea mpango mkakati wa kuhakikisha tunajenga timu imara.

Aidha Mwakilishi wa wachezaji kutoka  timu ya Ihefu Morice Chuku amesema kuwa  wamejipanga kuhakikisha wanawafurahisha mashabiki wao kwani wapo katika uwanja wa nyumbani  na tunawaomba wajitokeze kwa wingi kuisapoti timu yao.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments