UTEKELEZAJI WA ILANI YA CHAMA CHA MAPINDIZU SAMBAMBA NA UKAGUZI WA MIRADI KATA YA MIKOCHENI.

 

Chama cha mapinduzi Kata ya Mikocheni kimefanya zoezi la utekelezaji wa ilani kwa kutembelea miradi inayotekelezwa katika kata hiyo. 

Ziara hiyo imeongozwa na Diwani wa Kata hiyo Eng Zenzely Hussen Iddy akiambatana na watendaji wa Kata,Mitaa na Viongozi wa Kamati Mbalimbali wa Chama cha Mapinduzi. 


Diwani wa Kata ya Mikocheni Eng Nzenzely Hussein katikaki wakiwa kwenye ukaguzi wa miradi ndani ya Kata ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Chama. 

Hamisi Malela Mwalimu Mkuu wa shule hiyo amezungumza kwaniaba ya Wanafunzi na Walimu wa shule amesema kujengwa kwa maabara kutaongeza ufaulu kwasababu shule hiyo inafanya vizuri katika masomo ya sayansi wakiwa hawana maabara wanatumia madarasa. 

Pia Eng Angel Michese msimamizi wa mradi huo amesema ujenzi unaendelea vizuri mpaka kufikia mwezi wa kwanza mradi utakuwa umekamilika. 

Mradi wa vyumba vya madarasa ya Ghorofa na Maabara tatu (3) Kemia, Fizikia na Baiolojia shule ya sekondari Mikocheni. 

Sanjari na mradi huo pia wambelea mradi wa barabara ya Regent ambao umekamilika kwa kiwango cha lami na kugharimu zaidi ya shilingi milioni 676 yenye urefu wa km 0.64. 

Pichani barabara ya regent iliyo kamilika kwa kiwango cha lami. 

Vilevile wametembelea barabara ya chwaku yenye urefu wa km 0.6 kwa kiwango cha lami utekelezaji unaendelea kukamilisha mradi huo. 

Pichani barabara ya Chwaku ikiwa katika matengenezo. 

Aidha walitembelea mradi wa kisima cha maji ulipo Mikocheni À ambao unajumisha jumla ya visima kumi na sita vilivyo jengwa katika kata hiyo ambavyo vimepunguza hadha ya upatikanaji wa maji ambao ulikuwa changamoto kwenye kata hiyo. 

Mradi wa kisima cha maji uliopo mikocheni mtaa wa darajani kilichofaziliwa na YilmazMehmet Ali Dertop. 

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments